Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI aliuliza: - Je, Serikali inaichukulia hatua gani TARURA Msalala kwa kuchelewesha mikataba na kuwapa kazi wakandarasi wasio na uwezo?

Supplementary Question 1

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza nasikitika kwa kupata majibu ambayo sio; niseme tu kwa lugha nyepesi kwamba siyo ya ukweli. Barabara haziwezi zikakosa wakandarasi.

Mheshimiwa Spika, naomba sasa niulize maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa kumekuwa na kucheleweshwa kwa mikataba hiyo juu ya kuwepo taratibu nyingi za manunuzi: Je, Serikali ina mkakati gani sasa wa kupunguza milolongo hiyo ya manunuzi ili mikataba hii iweze kusainiwa kwa wakati? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, ni lini sasa Serikali itaanzisha au itarudisha mfumo wa kila Halmashauri kuwa na Meneja wa TARURA? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Iddi Kassim Iddi, Mbunge wa Jimbo la Msalala kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza tu nimweleze Mheshimiwa Mbunge kwamba taratibu za manunuzi kwenye kandarasi zozote tunazozifanya ni lazima zifuatwe. Nasi hatutaruhusu mtu yeyote kukiuka hizi taratibu za kimanunuzi. Kikubwa tu ni kwamba tunaendelea kuboresha mifumo ili kuhakikisha kwamba tenda zote zinazotangazwa ziweze kupatikana kwa muda ili kazi ambazo zimekusudiwa zifanyike kwa haraka. Kwa hiyo, tumekuwa tukiboresha na ndiyo maana sasa hivi watu wote wanaomba kupitia mfumo.

Mheshimiwa Spika, la pili, utaratibu uliopo sasa ni kwamba kila Halmashauri tumeweka Meneja wa TARURA ambaye anasimamia barabara katika eneo lake. Ahsante.

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI aliuliza: - Je, Serikali inaichukulia hatua gani TARURA Msalala kwa kuchelewesha mikataba na kuwapa kazi wakandarasi wasio na uwezo?

Supplementary Question 2

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Eneo la Mto Mori linalounganisha Kata nne Kata ya Nyabulongo, Nyatorogo, Kigunga na Milale ni eneo ambalo wananchi wamekuwa wakipoteza maisha kwa muda mrefu sana hasa pale wanapojaribu kuvuka kutoka upande mmoja kwenda upande mwingine. Hivi ninavyozungumza, wananchi watano wamefariki na mpaka sasa tunaendelea na maombolezo ambapo walijaribu kuvuka kwa kutumia vyombo kwenye eneo lile.

Mheshimiwa Spika, nilitaka nijue Serikali ina mpango gani wa kutengeneza mkataba wa dharura angalau kwa kujengewa daraja kwa kutumia mkataba wa dharura ili kunusuru maisha ya hawa wananchi ambao hawana namna, wanalazimika kuvuka kwenda upande wa pili kutafuta huduma za kijamii? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Jafari Chege, Mbunge wa Rorya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, bahati nzuri jambo ambalo amelieleza Mheshimiwa Mbunge ninalifahamu. Nasi tumeshamwagiza Mtendaji Mkuu wa TARURA kupeleka timu ya kwenda kufanya tathmini na baada ya hapo, watatuletea taarifa ili sasa tuandae mchoro kwa ajili ya ujenzi wa daraja la kudumu katika eneo hilo. Tathmini ya awali ambayo tafanyika sasa, itapelekea sasa angalau tuweke kivuko cha muda wa dharura ili wananchi wale waweze kuvuka katika eneo hilo. Ahsante sana.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI aliuliza: - Je, Serikali inaichukulia hatua gani TARURA Msalala kwa kuchelewesha mikataba na kuwapa kazi wakandarasi wasio na uwezo?

Supplementary Question 3

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa Waziri Mkuu alifanya ziara pale Wilayani Nyang’hwale na akatoa ahadi ya ujenzi wa kilometa mbili Makao Makuu ya Wilaya; na Mheshimiwa Waziri Silinde alikuja pale akajionea lile vumbi ambalo linatimka pale katikati ya mji: -

Je, ni lini Serikali itajenga ama kukamilisha ahadi ya Waziri Mkuu? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hussein Amar, Mbunge wa Jimbo la Nyang’hwale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli mimi nimefika pale na ni kweli kabisa kwamba kuna ahadi ya Mheshimiwa Waziri Mkuu. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba ahadi za viongozi wakuu ikiwemo ya Waziri Mkuu ambayo ameitoa, itatekelezeka kwa vitendo. Kwa hiyo, nimwondoe shaka na bahati nzuri nafahamu lile eneo. Kwa hiyo, lipo katika mpango wetu, tumeliweka, na tutalifanyia kazi. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI aliuliza: - Je, Serikali inaichukulia hatua gani TARURA Msalala kwa kuchelewesha mikataba na kuwapa kazi wakandarasi wasio na uwezo?

Supplementary Question 4

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa kuwa kumekuwa na baadhi ya wakandarasi ambao wanaacha madeni kwa wananchi kwa kazi za kujitolea na kokoto: Nini kauli ya Serikali kwa wananchi hawa wanaoachwa na madeni na Mameneja wa TARURA kuzuia hili lisitokee siku nyingine?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Olelekaita, Mbunge wa Kiteto, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli tumekuwa tukipata hiyo changamoto na tumekuwa tukielezwa na wananchi katika maeneo mbalimbali kwamba wakandarasi wamekuwa wakiacha hayo madeni katika maeneo husika. Moja ya utaratibu wetu sasa hivi, kabla ya kumaliza ule mkataba, hatutalipa fedha zote za mwisho mpaka pale ambapo watakuwa wamemaliza madeni ya watu katika maeneo husika. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI aliuliza: - Je, Serikali inaichukulia hatua gani TARURA Msalala kwa kuchelewesha mikataba na kuwapa kazi wakandarasi wasio na uwezo?

Supplementary Question 5

MHE. YAHYA A. MHATA: Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri Mkuu mwaka 2018 aliahidi kujenga kilometa tano za lami ndani ya Mji wa Mangaka katika Wilaya yangu ya Nanyumbu: -

Je, ni lini ahadi hii ya kiongozi wetu itatekelezwa ndani ya wilaya yangu?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Mhata, Mbunge wa Nanyumbu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nilijibu swali la awali la Mheshimiwa Hussein Amar, Mbunge wa Nyang’hwale, ndivyo ambavyo naweza kumwambia Mheshimiwa Mbunge kwamba ahadi zote zipo katika mpango wetu na bahati nzuri Bunge lako Tukufu kupitia kauli ya Mheshimiwa Rais mlituongezea fedha Ofisi ya Rais ya TARURA.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, sasa hivi angalau tuna wigo mpana wa kuhakikisha kwamba tunatekeleza hizi ahadi za viongozi kwa wakati. Kwa hiyo, nimwondoe wasiwasi kwamba kabla ya mwaka 2025 tutakuwa tumeanza utekelezaji wa ahadi hiyo ya Waziri Mkuu. Ahsante sana.