Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Salim Mussa Omar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Gando

Primary Question

MHE. SALIM MUSSA OMAR aliuliza: - Je, kuna Mwongozo unaosema kuwa Zanzibar Insurance Corporation haipaswi kushiriki kukata Bima za Miradi mikubwa?

Supplementary Question 1

MHE. SALIM MUSSA OMAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa hii ya kuweza kuuliza swali la nyongeza. Kumekuwa na malalamiko makubwa ya kukoseshwa fursa ZIC kama fursa inayopatikana na NIC huku Tanzania Bara: -

Je, Serikali inatuhakikishia vipi kwamba kuna mchakato sasa kuweza kuondoa malalamiko haya ili sasa Zanzibar insurance kwa sababu ipo katika mikoa zaidi ya mitano huku Tanzania Bara inaweza ikapewa fursa sawa kuweza kuingia katika miradi mikubwa ya Tanzania Bara?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mussa Omar Salim, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nimejibu kwenye jibu langu la msingi kwamba ZIC ni kampuni kama makampuni mengine. Kazi ya Serikali ni kuhakikisha kwamba inaweka mazingira rafiki ya kiushindani na kuhakikisha kwamba wanaweza kufanya biashara bila kuwa na changamoto yoyote.

Mheshimiwa Naibu Spika, naamini kabisa kwamba Serikali ikishaweka mazingira hayo, basi hata wao watajipima kulingana na mazingira ya kiushindani, kwa sababu kwa mujibu wa Sheria Serikali haiwezi kuingilia biashara ambazo wadau wanaweza kushiriki kwa pamoja. Ahsante.

Name

Najma Murtaza Giga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SALIM MUSSA OMAR aliuliza: - Je, kuna Mwongozo unaosema kuwa Zanzibar Insurance Corporation haipaswi kushiriki kukata Bima za Miradi mikubwa?

Supplementary Question 2

MHE. NAJMA MURTAZA GIGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nami nilikuwa na swali la nyongeza. Kumekuwa na matangazo kwa ajili ya kulifagilia Shirika la Bima la Taifa kwamba mashirika mengi ya Umma yatumie shirika hili kwa sababu ni la Umma. Hata hivyo, tukizingatia pia Shirika la Bima la Zanzibar ni Shirika la Umma pia, na tumeambiwa kwamba ni biashara huria: Kwanini na ZIC nayo isitangazwe kama ambavyo inatangazwa NIC ili iweze kufanya kazi sawa? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Najma, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema katika majibu yangu ya msingi ni kwamba mashirika ambayo yanasajiliwa kwa mfumo ya kampuni yanaendeshwa kwa mujibu wa sheria za kikampuni na sheria za kiushindani.

Kwa hiyo, sisi kama Serikali, iwapo kunakuwa na changamoto yoyote ile, basi tutaendelea kufanya utafiti na kujiridhisha ili njia stahiki sichukuliwe kuhakikisha kwamba mashirika haya ambayo ni moja ya Mashirika ya Umma pia tuweze kuona kwamba ni mazingira yapi yatawezesha kujiendesha kibiashara zaidi. Ahsante.