Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUDITH S. KAPINGA aliuliza: - Je, Serikali kupitia Tume ya Ushindani (FCC) ina mkakati gani wa kumlinda mlaji katika biashara za mtandaoni?

Supplementary Question 1

MHE. JUDITH S. KAPINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naishukuru Serikali kwa mujibu mazuri. Suala la ulinzi wa mlaji kwenye biashara za kimtandao hauwezi kusubiri Mpango Mkakati wa Miaka Mitano kwa sababu tayari tumechelewa na hivyo madhara makubwa yanaonekana kwa walaji pamoja na wafanyabiashara.

Je, Serikali haioni umuhimu wa kufanya utaratibu wa haraka labda kwa kuweka kanuni ili kuweza kumnufaisha mfanyabiashara huyu na mlaji katika mitandao hii ya kijamii? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Judith Kapinga Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia sana kuhusu biashara na hasa biashara mtandaoni. Ni kweli tuna mkakati huo lakini hatuwezi kusubiri mkakati ili tuweze kutelekeza majukumu ya kumlinda mlaji kwa sababu biashara mtandaoni ziandelea. Ndiyo maana sasa tunafanya marekebisho ya Sheria ya Ushindani Na. 8 ya Mwaka 2003 ambayo pia ina jukumu la kumlinda mlaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zaidi tumeshachukua hatua zaidi, tumeanza kuhamasisha biashara mtandaoni na Waheshimiwa Wabunge watakumbuka mwaka 2021 wakati wa Maonesho ya Saba Saba tumefungua biashara mtandaoni kupitia Shirika letu la Posta; Posta hii ya commerce na mambo mengi yanafanyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hatuwezi kusubiri mkakati, kuna jitihada nyingi zinaendelea wakati pia na hili la mkakati linaendelea kufanyika ili kuhakikisha tuna uhakika wa kuwalinda walaji wanaotumia biashara mtandaoni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.