Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza vyanzo vya mitaji kwa akina Mama wajasiriamali mbali ya fedha zinazotolewa na Halmashauri?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwanza kabisa nimshukuru Naibu Waziri kwa majibu mazuri. Nimpongeze Mheshimiwa Rais kwa kufuta riba kwa mkopo wa asilimia 10 kwa wanawake.

Mheshimiwa Spika, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa wanawake wengi ni waaminifu sana katika masuala ya kurudisha mikopo, Je Serikali ina mpango gani wa kuongeza muda wa marejesho? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili kwa kuwa mahitaji ya mikopo ni mengi kwa wanawake, vijana na walemavu. Je, Serikali au Wizara ina mpango gani wa kuongeza asilimia 15, asilimia Saba wakopeshwe wanawake, asilimia Tano wakopeshwe vijana, asilimia Tatu watu wenye ulemavu? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Esther Midimu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nichukue nafasi hii kumshukuru sana na kumpongeza Mheshimiwa Esther Midimu kwa kufuatilia kwa makini sana kuhusiana na maendeleo ya wanawake na hasa kushiriki katika shughuli za kiuchumi kupitia ujasiriamali.

Mheshimiwa Spika, ni kweli Serikali imekuwa ikifanya juhudi mbalimbali kama nilivyosema kwa kuanzisha mifuko pia kwa kuweka mfuko maalum ambapo kuna Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake, pia mfuko wa asilimia 10 zinazotengwa katika Halmashauri lakini pia kupitia taasisi za fedha nyingine zinazolenga kuhudumia makundi mbalimbali yakiwemo wanawake.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tunaendelea kuongeza fedha kwa namna tofauti tofauti ili kuhakikisha wanawake wanashiriki kikamilifu katika kuongeza uchumi wa nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuhusu hitaji la pili nipende kumshukuru Mheshimiwa Esther kwamba ametoa mawazo ya kuona namna gani Serikali itaongeza asilimia kutoka zile asilimia 10 zinazotengwa katika Halmashauri kwenda asilimia 15. Nadhani hili ni suala zuri tunalichukua ili kulifanyia kazi pamoja na wenzetu wa TAMISEMI. Nakushukuru sana. (Makofi)