Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE aliuliza: - Je, ni lini Barabara inayounganisha Wilaya ya Kyela na Ludewa kupitia Matema, Ikombe mpaka Liuli itaanza kujengwa?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Spika, Kijiji cha Ikombe, tangu kuumbwa kwa dunia hii hawajawahi kuona gari. Zimebaki kilomita moja na nusu, ili barabara ifunguke mpaka Kijiji cha Ikombe, na mwezi wa kumi tuliambiwa kwamba mkandarasi yuko tayari, amepatikana.

Je, Mheshimiwa Waziri anajua kwamba mkandarasi mpaka sasa hivi hayuko site?

Mheshimiwa Spika, mbili, barabara ya Ngamanga – Lusungo Matema inaenda moja kwa moja Ikombe, pale kuna daraja la bilioni 4.50 lakini eneo la Ngolwa halina daraja. Je, unaonaje sasa ni wakati sahihi wa kujenga daraja la Ngorwa, ili barabara ipitike kirahisi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFRY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya mheshimiwa Ally Anyingulile Jumbe Mlaghila, Mbunge wa Kyela kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba wananchi ambao hawajaona gari nimuhakikishie kwamba barabara hiyo tunaifikisha kwenye hicho kijiji ili wananchi hao waweze kuiona gari katika maisha yao.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, naomba nichukue nafasi hii kumuagiza Meneja wa Mkoa wa Mbeya, ahakikishe kwamba mkandarasi anarudi site na anafanya kazi ambayo anatakiwa kuifanya. Lakini kuhusu daraja hili ambalo amelisema, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali italijenga hili daraja ili paweze kuwa na mawasiliano ambayo yamekosekana kwa sasa. Ahsante.

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE aliuliza: - Je, ni lini Barabara inayounganisha Wilaya ya Kyela na Ludewa kupitia Matema, Ikombe mpaka Liuli itaanza kujengwa?

Supplementary Question 2

MHE. JUDITH S. KAPINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Je, ni lini barabara ya kutoka Tanga, Mkumbi, Lugali inayoenda kuunganika na barabara ya Lutoho, Nyasa yenye takribani kilomita 18 itajengwa kwa kiwango cha lami, ikizingatia imekuwa na adha kubwa za kiuchumi kwa wananchi wa maeneo hayo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFRY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kapinga, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoainisha ni kweli ipo na imeahidiwa na ipo hata kwenye ilani. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii itajengwa kwa kiwango cha lami kulingana na upatikanaji wa fedha. Ahsante.

Name

Jonas William Mbunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE aliuliza: - Je, ni lini Barabara inayounganisha Wilaya ya Kyela na Ludewa kupitia Matema, Ikombe mpaka Liuli itaanza kujengwa?

Supplementary Question 3

MHE. JONAS W. MBUNDA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Barabara ya Mbinga, Litembo, Kili ilitolewa ahadi na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Nilitaka nijue je, Serikali ina mpango gani wa kuanza kujenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFRY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunda Mbunge wa Mbinga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ahadi zote ambazo zimetolewa na Waheshimiwa viongozi wakuu wa nchi, ni ahadi ambazo tunazitekeleza. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunda, Mbunge wa Mbinga, kwamba barabara hii ipo kwenye mpango kwa ajili ya kuijenga kama ambavyo viongozi wetu walioahidi na sisi tutamhakikishia kwamba ahadi hiyo tutaitekeleza.

Name

Dr. Joseph Kizito Mhagama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Madaba

Primary Question

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE aliuliza: - Je, ni lini Barabara inayounganisha Wilaya ya Kyela na Ludewa kupitia Matema, Ikombe mpaka Liuli itaanza kujengwa?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. JOSEPH K. MHAGAMA: Mheshimiwa Spika, ahsante, wananchi wa Jimbo la Madaba, na wananchi wa Ludewa wamesubiri kwa hamu sana ujenzi wa Barabara ya Mababa – Mkiu – Ludewa kwa kiwango cha lami na hii imekuwa ahadi ya kudumu ya Serikali. Ni lini sasa Serikali itatekeleza azma hii?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFRY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Mhagama, Mbunge wa Madaba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Mkiu kwenda Madaba ni barabara ambayo inaanzia Itoni, Lusitu, Mkiu kwenda Madaba ambayo ndiyo inaenda kwenye madini ya chum ana makaa ya mawe. Usanifu ulishakamilika kwa kipande cha Mkiu kwenda Luhuu hadi Madaba, Serikali inaendelea kutafuta fedha sasa kuianza kuijenga kwa kiwango cha lami. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hiyo itajengwa kwa sababu pia ni barabara muhimu sana kwa uchumi wa nchi yetu ya Tanzania, Ahsante. (Makofi)

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE aliuliza: - Je, ni lini Barabara inayounganisha Wilaya ya Kyela na Ludewa kupitia Matema, Ikombe mpaka Liuli itaanza kujengwa?

Supplementary Question 5

MHE. STELLA S. FIYAO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Nataka kujua ni lini Serikali itaanza upanuzi wa barabara kutoka Mpemba mpaka Tunduma – Transfoma ili kuepusha changamoto ambayo wananchi wamekuwa wakiipata kutokana mlundikano na msongamano mkubwa wa magari makubwa ambayo yamekuwa yakivuka mpaka wa Tanzania?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFRY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Stella Fiyao, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Songwe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja imeshafanyiwa usanifu na ni sehemu ya barabara ya kuanzia Igawa – Mbeya hadi Tunduma. Na barabara hii kipande cha Mpemba hadi Tunduma kitapanuliwa kuwa njia nne. Kwa hiyo iko kwenye mpango na tunategemea mwaka ujao wa fedha tutaanza kupanua hii barabara kuwa njia nne ili kupunguza msongamano ambao upo katika mji wa Tunduma. Ahsante.

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE aliuliza: - Je, ni lini Barabara inayounganisha Wilaya ya Kyela na Ludewa kupitia Matema, Ikombe mpaka Liuli itaanza kujengwa?

Supplementary Question 6

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Spika, nauliza je ni lini barabara ya kuunganisha kutoka Mbambay hadi Ludewa itajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFRY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Thea Ntara, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara inayotokea Mbambay Wilaya ya Nyasa kuja Litui na kuvuka daraja la Luhuu tayari tumeshakamilisha daraja na usanifu umeshakamilika kati ya Mbambay hadi Litui, fedha inatafutwa ili sasa tuanze kuijenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, ahsante.