Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Simon Songe Lusengekile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Chuo cha VETA katika Halmashauri ya Wilaya ya Busega?

Supplementary Question 1

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE: Mheshimiwa Spika, kwanza niishukuru sana Serikali kwa kutenga fedha, lakini pia nimshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kupeleka fedha wilayani kama alivyotuhakikishua Mheshimiwa Naibu Waziri. Sasa nina maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa Serikali sasa imesema miradi hii ya ujenzi wa vyuo vya VETA itaanza mwaka huu kwa Wilaya 63 ikiwemo na wilaya ya Busega. Je, nini mpango wa Serikali wa kumaliza vyuo hivyo kwamba itamaliza lini ili Watanzania waweze kunufaika katika hizi Wilaya 63?

Swali la pili, je Naibu Waziri yuko tayari sasa kutembelea Busega ili tuje tumuoneshe eneo ambalo tayari tumeshatenga kwa ajili ya ujenzi wa VETA?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Simon Songe, Mbunge wa Busega kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyokwishaeleza kwenye majibu ya msingi kwamba Serikali imetenga fedha na tunaenda kuanza ujenzi huu baada ya taratibu za manunuzi, lakini topographical survey, geo-technical survey pamoja na environment impact assessment kuweza kukamilika. Kwa hiyo nimuondoe hofu na wasiwasi kwamba tunaenda kuanza ujenzi huu.

Mheshimiwa Spika, lakini lini tutamaliza? Kwanza naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ujenzi huu tutajenga kwa awamu, kwa hiyo katika awamu ya kwanza tunakwenda kujenga majengo tisa ikiwemo na karakana tatu, lakini katika awmu ya pili tunakwenda kujenga majengo nane ili kuweza kukamilisha yale majengo 17.

Kwa hiyo, katika mwaka huu wa fedha tutakadiria kwamba au tunaazimia tutakamilisha yale majengo tisa na katika mwaka ujao wa fedha tutamalizia yale majengo manane yaliyobaki. Kwa hiyo, matarajio ya kumaliza ni mpaka mwaka ujao wa fedha tutakapokamilisha majengo yote 17.

Mheshimiwa Spika, katika swali la pili ameulizia kuhusu suala la kwenda. Hili ni jukumu letu, ni kazi yetu kwa vile tunapeleka fedha kule, fedha nyingi, ni lazima tufanye usimamizi wa karibu na ufuatiliaji wa karibu. Kwa hiyo tuko tayari kama Wizara kwenda kuona maeneo haya ya ujenzi, lakini vilevile kwenda kuratibu taratibu za ujenzi kuhakikisha kwamba unakamilika kwa viwango vinavyohitajika, nakushukuru sana.

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Chuo cha VETA katika Halmashauri ya Wilaya ya Busega?

Supplementary Question 2

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Kilwa ni miongoni mwa wilaya zitakazonufaika na mradi wa ujenzi wa vyuo 63 vya VETA, tumeshaandaa eneo katika Kitongoji cha Matapatapa Kijiji cha Njia Nne na pia tumewekeza shilingi milioni 6.5 kwa ajili ya uandaaji wa hati pamoja na kufanya environmental impact assessment.

Je, ni lini ujenzi wa chuo hicho utaanza?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Ndulane, Mbunge wa Kilwa Kaskazini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyozungumza kwenye majibu ya msingi kwamba tutakapokamilisha tu taratibu za manunuzi pamoja na hizi geo-technical, topographical pamoja na environmental impact assessment tunatarajia kuanza. Matarajio yetu kunako kuanzia mwezi wa nne hivi tuweze kuanza ujenzi huu katika maeneo yote nchini. (Makofi)

Name

Nicholaus George Ngassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Chuo cha VETA katika Halmashauri ya Wilaya ya Busega?

Supplementary Question 3

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, Serikali imekamilisha ujenzi wa Chuo cha Mafunzo ya Ufundi Stadi - VETA kwenye Jimbo la Igunga.

Swali langu kwa Serikali; je, ni lini Serikali itafanya udahili na kuanza kwa wanafanzi kusajiliwa? Ahsante.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Nicholaus Mbunge wa Igunga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza tulikuwa hatujakamilisha ujenzi kwa asilimia 100, Mheshimiwa Rais mwezi wa kumi na mbili alitoa fedha saidi ya shilingi bilioni 10.3 kwa ajili ya umaliziaji wa vile vyuo 25, fedha hizo tayari tumeshazipeleka kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo na pale Igunga. Kwa hiyo, ujenzi sasa tunaenda kukamilisha na tunatarajia kuanzia mwezi wa nne tuanza kudahili zile kozi za muda mfupi, nashukuru sana.

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Chuo cha VETA katika Halmashauri ya Wilaya ya Busega?

Supplementary Question 4

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Spika,nakushukuru kwa kunipatia nafasi.

Ni lini Serikali itajenga karakana ngumu katika Chuo cha VETA kitangali karakana ngumu ambazo ni uselemala na welding kwa sababu karakana hizo hazipo katika chuo hicho? Ahsante.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Maimuna Mtanda, Mbunge wa Newala kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli katika chuo chetu cha Kitangali kuna upungufu wa karakana na mimi nilishafika pale, nilifanya ziara mwaka jana kuweza kwenda kuona eneo lile na nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge katika bajeti tutakayoiandaa ya mwaka 2023/2024 tunakusudia kuhakikisha kwamba maeneo yale ambayo kuna upungufu wa karakana ikiwemo pale Kitangali pamoja na Mikumi kwa Mheshimiwa Londo tunatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa karakana kwenye maeneo hayo.

Name

Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Chuo cha VETA katika Halmashauri ya Wilaya ya Busega?

Supplementary Question 5

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru na mimi nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Chuo cha Ufundi VETA Wilaya ya Chemba kimekamilika zaidi ya asilimia 80; ni lini sasa Serikali itaanza kudahili kwa kozi hizo ndogo ndogo za muda mfupi kwa maana miwili/miezi mitatu ili vijana wetu walipo mitaani waondokane na adha ya ajira na hatimaye waweze kujiajiri? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Kunti Majala, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyoeleza kwenye swali la Mheshimiwa Ndulane, Chuo cha Chemba ni miongoni mwa vile vyuo 25 ambavyo vilikuwa bado havijakamilika. Kwa hiyo, kuna snag ndogo ndogo ambazo zilikuwa za kumalizia. Zaidi ya shilingi milioni 400 ilikuwa inahitajika na Mheshimiwa Rais tayari ameshatoa fedha zaidi ya shilingi bilioni 10.3 kwa ajili ya ukamilishaji wa vyuo hivi 25. Tayari fedha hizi tumeshazipeleka pale Chemba na maeneo mengine na tunatarajia kuanzia mwezi wa nne kozi hizi za muda mfupi tuweze kuanza kudahili na ziweze kutolewa katika maeneo ya Chemba na maeneo mengine vyuo hivi 25 vinapojengwa.