Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatambua mipaka ya Halmashauri ya Mkalama na Iramba ili kuondoa migogoro katika Kata za Tumuli, Kinyangiri na Gumanga?

Supplementary Question 1

MHE. FRANCIS I. MTINGA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri sana ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, naomba nimtake Waziri, pamoja na kwamba wataalamu wamefanya mambo haya, lakini Wakuu wa Wilaya walipaswa Kwenda kufanya mkutano pale kwa pande zote mbili na kuonesha beacon, lakini jambo hilo halijafanyika.

Je, uko tayari sasa kuwataka Wakuu wa Wilaya kwa muda maalum kwenda kutekelza agizo hili?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa jimbo langu linapakana pia na Mkoa wa Simiyu na Mkoa wa Manyara na tatizo hili mipaka limekuwa kubwa.

Je, agizo hilo pia utamwagiza pia Mkuu wa Mkoa wa Singida na Mkuu wa Mkoa wa Manyara kwenda kufanya mambo haya haya ili tatizo hili liweze kuisha? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Francis Isack Mtinga, Mbunge wa Jimbo la Iramba Mashariki ama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza nitoe rai kwa Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya hizi na Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa, kama ambavyo maelekezo ya Serikali siku zote yamekuwa yakitolewa kwamba ni muhimu na ni lazima kufika katika maeneo yenye migogoro ya mipaka kati ya kijiji na kijiji, kata na kata lakini kati ya wilaya na wilaya na mkoa na mkoa, ili kuhakikisha kwamba tunatatua changamoto za mipaka kwa kutumia njia shirikishi na kuhakikisha kwamba wananchi wanaendelea kuishi kwa amani na utulivu.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naelekeza Wakuu wa Wilaya hizi na Mikoa ya Manyara lakini na Singida kuhakikisha kwamba wanatekelza haya maelekezo ya Serikali, ahsante.