Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Alice Karungi Kaijage

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kutoa elimu kwa watumishi juu ya ukokotoaji wa mafao?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa katika formula ya kikokotoo kilichopita watumishi wengi walikwishakopa na wanaostafu sasa hivi walikwishakopa sana.

Je, Serikali ilishaliona hili jambo kwamba hatma yao ni nini, kwa sababu kikokotoo cha sasa kimekuja na formula nyingine ambayo wanatoka kana kwamba mafao yao ni zaidi ya nusu hawajapata?

Je, Serikali ilishafikiria jambo hili na nini hatima ya Watumishi hawa ambao mafao yao yalishaiva na walishakopa kupitia formula iliyopita?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Spika, ahsante, kabla ya kufanya uamuzi huo, mchakato huu ulishirikisha wadau wote na kuliandaliwa actuarial report. Katika kufanya hivyo tulibaini mambo kama hayo ambayo Mheshimiwa Mbunge amesema na nimpongeze sana kwa kuendelea kuwa mfuatiliaji mzuri.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Serikali wakati wa kufanya hivyo, kikokotoo kipya kimesaidia kuja kuongeza lile pato la kila mwezi. Ni tofauti hata na kikokotoo kile cha awali ambacho hakikuweza kuleta tija zaidi.

Kwa hiyo, mengine kwa sababu ndio tumekwisha anza na sheria zetu zimekwisha anza, hakuna ule msingi wa retrospectivity kwa maana ya sheria kuanza kufanya kazi kwenda mbele na sio kurudi nyuma. Tutazidi kuyazingatia yote hayo na changamoto ndogo ndogo zinazojitokeza ili kuweza kuhakikisha jambo hili linaleta maslahi makubwa kwa wafanyakazi na tija, kwa sababu Serikali inaheshimu sana nguvu kazi ya Taifa ambayo ndiyo inaweza kuleta maendeleo endelevu kwa ajili ya taifa letu, ahsante sana.