Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo la maji kwenye Mji Mdogo wa Laela na Mpui katika Jimbo la Kwela?

Supplementary Question 1

MHE. DEUS C. SANGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa nafasi ya maswali madogo ya nyongeza.

Swali langu la kwanza, kwanza niipongeze Serikali kwa nia ya dhati ya kutatua kero kwenye Mji wa Mpui na Laela kwa kutumia chanzo cha Ziwa Tanganyika na Mto Momba.

Je, ni lini mkandarasi anayefnaya Mradi wa Kaoze Group ataripoti kuanza kazi kwenye Kata ya Kaoze, Kilanga One na Kipeta?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; kwa kuwa tatizo la maji kwenye Mji Mdogo wa Mpui ni kubwa sana na mmesema mnaenda kuchimba kisima kimoja.

Je, Serikali hamuoni kuna haja ya kuendeleza mpango wenu wa kutumia Mto Kazila kupeleka maji katika Mji Mdogo wa Mpui?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Deus Sangu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimepokea pongezi, nikupongeze nawe pia kwa sababu ufuatiliaji wako katika suala hili umekuwa ni mzuri.
Mheshimiwa Spika, lini mkandarasi atakwenda, ni mwezi wa tatu mwanzoni; wiki ya kwanza ya mwezi wa tatu tunatarajia mkandarasi huyu atafika site na kuanza kazi ya mradi.

Mheshimiwa Spika, matumizi ya Mto Kazila, ni kweli usanifu ulifanyika. Mto huu upo mbali kodogo wa kilometa 21 na ipo kwenye Wilaya tofauti na ambapo mradi upo. Kwa hiyo, tutachimba kisima kwa sababu tuna uhakika tutapata maji ya kutosha kama tulivyochimba maeneo mengine katika jimbo lako Mheshimiwa Mbunge. Itakapobidi kutumia Mto Kazila kwa sababu Wizara tunahitaji kuona tunatumia vyanzo vyote ambavyo vinatuletea miradi endelevu, Mto Kazila pia tutautumia.

Name

Hamis Mohamed Mwinjuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo la maji kwenye Mji Mdogo wa Laela na Mpui katika Jimbo la Kwela?

Supplementary Question 2

MHE. HAMIS M. MWINJUMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Tatizo la upatikanaji wa maji katika Mji wa Muheza bado ni kubwa pamoja na juhudi nyingi zinazofanywa na Serikali.

Je, ni lini mradi wa miji 28 ambao tunaamini kwamba ndiyo suluhisho la kudumu la tatizo hili utaanza kutekelezwa?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hamis, Mbunge wa Muheza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mradi wa Miji 28; miradi hii yote imeshaanza kutekelezwa kwa hatua za awali za kukusanya taarifa na kukamilisha taratibu za kuanza ujenzi tayari zimeshaanza ni vile hamzioni wanakusanya taarifa. Mradi huu ni design and build, kwa hiyo mwezi huu wa tatu tunatarajia wakandarasi waanze kuonekana sasa site na kuanza kufanya ujenzi.

Name

Sylivia Francis Sigula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo la maji kwenye Mji Mdogo wa Laela na Mpui katika Jimbo la Kwela?

Supplementary Question 3

MHE. SYLVIA F. SIGULA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa wananchi wa Kigoma Mjini wameahidiwa mradi mkubwa wa maji kukamilika tangu mwaka 2020 na sasa tuko mwaka 2023 na mradi haujakamilika.

Je, ni nini kauli ya Serikali kwa wananchi wa Kigoma Mjini kuhusu mradi huo mkubwa?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sylvia, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mradi Kigoma Mjini, mimi mwenyewe nimefika mwezi Novemba, mradi upo kwenye hatua za mwisho kabisa na maji yataanza kutoka hivi punde.

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo la maji kwenye Mji Mdogo wa Laela na Mpui katika Jimbo la Kwela?

Supplementary Question 4

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona.

Mheshimiwa Spika, katika Wilaya ya Kilwa, katika Vijiji vya Marendego na Kinjumbi kumekuwa na miradi ya maji ambayo imekuwa ikitekelezwa kwa zaidi ya miaka mitatu hivi sasa.

Ningependa kumuuliza Mheshimiwa Waziri kwamba ni lini miradi hii itakamilika ili wananchi wa vijiji hivyo waweze kupata huduma ya maji safi na salama?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Francis, Mbunge wa Kilwa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, vijiji hivyo ulivyovitaja Mheshimiwa Mbunge ni kweli kazi zimeendelea zikifanyika. Baada ya Bunge hili naomba tuwasiliane ili tuweze kuona tunafika pamoja katika miradi hii.

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo la maji kwenye Mji Mdogo wa Laela na Mpui katika Jimbo la Kwela?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. DAVID M. DAVID: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, ningependa kujua mradi mkubwa wa maji tambarare ya Mwanga mpaka Same unakamilika lini?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la Mheshimiwa David Mathayo, Mbunge wa Same kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mradi huu ni mradi mkubwa, utekelezaji wake unaendelea, pamoja na changamoto zake, Wizara inaendelea kuona tunafanya kila linalowezekana mradi uweze kukamilika na lengo la matumizi haya kwa wananchi wa Same, Mwanga mpaka Korogwe yaweze kukamilika.