Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Aleksia Asia Kamguna

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALEKSIA A. KAMGUNA aliuliza: - Je, Serikali imejipangaje kutoa elimu juu ya ugonjwa wa fistula?

Supplementary Question 1

MHE. ALEKSIA A. KAMGUNA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Katika Tanzania, ugonjwa huu wa fistula ni ugonjwa ambao unasumbua sana.

Je, ni hospitali ngapi au zipi zenye wataalamu wa kutibu ugonjwa wa fistula zilizoko nchini ukiondoa Hospitali ya CCBRT?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili. Ukiangalia sana ukizingatia haki za binadamu huu ugonjwa huwezi kumsafirisha mgonjwa kukiwa katika magari ya kawaida.

Je, Serikali imejipangaje kutoa usafiri maalum kwa ajili ya watu hao na namna ya kujikimu ili kutoka sehemu moja na kwenda nyingine ukizingatia waliowengi hali zao ni duni?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze kwa kufuatilia haya mambo ambayo kwa kweli yanawasumbua akina mama wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ameuliza ni hospitali ngapi; hospitali zetu zote za mikoa, kanda na taifa zinatoa huduma hiyo. Kumekuwepo kila wakati sasa hivi madaktari kutoka Hospitali ya Muhimbili na hospitali zetu za kanda wakienda kwenye hospitali za mikoa yetu ili kuendelea kuongeza nguvu na ujuzi kwa hospitali zetu za mikoa ili huduma hii iweze kutolewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa swali lake la pili; nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge; moja tuna mkakati kwamba magari yanapita kuhamasisha mtaani. Pia akipatikana mgonjwa yeyote huwa ambulance inamfuata na kupelekewa sehemu husika. Hata hivyo, ninajua kwamba kwenye eneo hilo bado hatujajiimarisha vizuri. Hivyo, tunachukua wazo lako ili tuweze kulifanyia karibu kwa kushirikiana na hospitali zetu za wilaya ili akina mama wale wakionekana waweze kupelekwa bila kupitia mabasi ya kawaida, waende kwa kutumia gari za Serikali.

Name

Maimuna Ahmad Pathan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALEKSIA A. KAMGUNA aliuliza: - Je, Serikali imejipangaje kutoa elimu juu ya ugonjwa wa fistula?

Supplementary Question 2

MHE. MAIMUNA A. PATHAN: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Tunajua ugonjwa huu unawasumbua akina mama wengi sana wakati wa kujifungua.

Je, Serikali haioni haja sasa ya kuongeza huduma za tija kwenye Hospitali za Mikoa ya Kusini?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBI WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Serikali inaongeza, na unapozungumzia kusini ndio maana kuna Hospitali ya Kanda ya Mtwara Kusini kule, ambayo kwa kweli inajengewa uwezo mkubwa kama hospitali zingine za kanda. Moja kutoa huduma lakini pia kujenga uwezo kwa hospitali za upande huu kwa chini ili waweze kutoa huduma hiyo. Pia kwa muda wa miaka hii miwili vimejengwa vituo 862; na kati ya hivyo 421 vimewekewa sehemu za kupasua akina mama ili kuwanusuru na hili jambo. Tutaendelea kufanya hivyo ili kuweza kuwanusuru akina mama. Kwa hiyo kuna mkakati wa nchi nzima si suala la Kusini peke yake.

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALEKSIA A. KAMGUNA aliuliza: - Je, Serikali imejipangaje kutoa elimu juu ya ugonjwa wa fistula?

Supplementary Question 3

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kama ilivyo ugonjwa wa fistula pia maambukizi ya virusi vya UKIMWI bado ni janga kwenye nchi yetu, lakini inaonekana kama Serikali imelegalega katika kutoa elimu. Mimi nataka kujua;

Je, ni nini mkakati wa Serikali kuendelea kutoa elimu ya kujikinga na virusi vya UKIMWI kwa wananchi wetu wa Tanzania?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBI WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nadhani anachosema, Serikali haijalegalega lakini ni strategy tu zimebadilika kwa ku-approach kulingana na hatua ambazo tumefikia. Kwa sababu ukiangalia hali ya maambukizi sasa hivi imeshuka sana na hali ya maambukizi ni makubwa kwa makundi maaulum na nguvu zinaelekezwa kwenye makundi maalum kuhakikisha hali hiyo inadhibitiwa.