Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza: - Je, ni lini Kijiji cha Kanonge Kata ya Nsimbo kitapelekewa umeme wa REA?

Supplementary Question 1

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikushukuru kwa kunipa nafasi hii. Hiki Kijiji cha Kanoge hata kwenye ramani ya REA hakipo, pamoja na vitongoji vyake. Sasa ninaomba uhakika kwa sababu nimetokea huko hata kwenye ramani ya REA, ina maana kijiji hiki ni kijiji cha siku nyingi, kilirukwa sasa naomba commitment ya Wizara. Ni lini kitawekwa kwenye ramani pamoja na vitongoji vyake na wataingia katika mchakato wa kuwekewa umeme?

Mheshimiwa mwenyekiti, la pili, katika Kijiji cha Usense Kata ya Ulwira pamoja na Kijiji cha Nyamasi, Kata ya Ugala mpaka leo miti inaoza hasa naomba commitment ya Wizara;

Je, ni lini vijiji hivyo vitapata umeme, kwa sababu hakuna dalili kabisa ya kupatiwa umeme? Ahsante.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Lupembe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye swali la pili nimuhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba, kabla ya mwaka huu kuisha, vijiji hivyo alivyovitaja ambavyo vinaonekana havijafikiwa na huduma ya umeme, vitakuwa vimefikiwa kwa sababu kwenye mkataba wetu tumekubaliana kabla ya Desemba mwaka huu vijiji hivyo viwe vimepata umeme na zile changamoto tulizokuwa nazo tayari tumezitatua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye swali la kwanza naomba nikitoka hapa nitawasiliana nae kwa sababu sisi taarifa tulizo nazo kutoka site ni hizi. Kwa hiyo tutakaa pamoja ili tuweze kuziweka pamoja. Niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge wote kwamba baada ya mradi wa REA-3 awamu ya pili kupita hatutarajii kuwepo na kijiji chochote ambacho hakina umeme; na hayo ndio maelekezo ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan. Kwa hiyo tutahakikisha rekodi zetu zinakaa sawa ili kila kijiji kiweze kuwa kimepata umeme kwa kadri ya mkataba na maelekezo yaliyopo.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza: - Je, ni lini Kijiji cha Kanonge Kata ya Nsimbo kitapelekewa umeme wa REA?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niulize swali dogo la nyongeza. Kijiji kidogo cha Msukanzi katika kata ya IIlula kimerukwa kuwekewa umeme lakini kata inayofuata kuna umeme. Sasa ni lini Serikali itaona umuhimu kwamba kuruka hivi vijiji si kitu kizuri, ili vijiji vyote viwe vinapata umeme kuliko kuacha kimoja hafu vingine vinapata?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ritta Kabati, Mbunge wa Viti Maalum, Iringa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuhakikishie yeye pamoja na Waheshimiwa Wabunge wote kwamba katika awamu hii ya tatu mzunguko wa pili ambayo ni ya mwisho hakuna kijiji kitakachoachwa. Tulipita humu Bungeni kwa Waheshimiwa Wabunge kuwaomba watuambie vijiji ambavyo vinadhani vimeachwa na tukavichukua tukaviweka kwenye orodha. Kwa hiyo kama kuna Mheshimiwa Mbunge yoyote anayedhani kuna kijiji ambacho kimerukwa kwa taarifa alizokuwa nazo basi tuwasiliane tukichukue kwa sababu sisi kwa taarifa tulivichukua vyote. Hata hivyo nitaenda pia kuwasiliana na Mheshimiwa Ritta Kabati, ili tukione hicho kijiji ambacho kimebaki tukichukue kama anavyosema.