Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza: - Je, kwa nini huduma za afya kwa Watoto Njiti zinatozwa fedha ilihali Sera ya Afya inaelekeza huduma bure kwa Watoto chini ya miaka mitano?

Supplementary Question 1

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mhesimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba niulize maswali madogo mawili. Kwa kuwa katika majibu ya msingi amesema matibabu ya wototo njiti hayatozwi, lakini kwa kuwa mpaka sasa huduma hizo zinatozwa;

Je, Serikali iko tayari kurejesha fedha ambazo wazazi waliojifungua watoto njiti walizitoa?

Kwa sababu ninayo madai ya mama anayedaiwa milioni moja na laki nane katika Hospitali ya Muhimbili.

Mhesimiwa Naibu Spika, kwa kuwa watoto njiti wamekuwa na changamoto mbali mbali za kiafya zinazowakosesha pengine kuendelea kuishi vema sawa sawa na watoto wengine;

Je, Serikali iko tayari kufanya mapitio ya likizo ya uzazi kwa wazazi wanaojifungua watoto njiti?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mhesimiwa Naibu Spika, nijibu maswali yake mawili kama ifuatavyo: -

Mhesimiwa Naibu Spika, moja; nitoe agizo kwa hospitali zote lakini vile vile mfuko wetu wa bima ya afya, kwamba suala la watoto njiti kama ni mama amejifungua na mtoto njiti au wakati wowote bima ya afya iweze kumuhudimia kama ni mwenye bima ya afya. Kuhusu kwamba wakizaliwa kwenye hospitali zetu zote watibiwe bure.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini Mheshimiwa Hokororo amesema je Serikali iko tayari kwa sababu ana ushahidi wa hospitali ambayo wanatoza. Ninakuomba Mheshimiwa Mbunge nikishakaa uje unionyeshe halafu tufuatilie nini kilichotokea. Siwezi kukuambia kwamba zitarudishwa lakini tutampata anayefanya hivyo na tuweze kumpa maelekezo mazuri, ili suala hilo lisijitokeze tena.

Mhesimiwa Naibu Spika, lakini la pili, suala la sheria ya likizo, hilo sasa ni la kisheria sio suala la Wizara ya Afya, lakini nimeshasikia kuna harakati hizo zinaendelea na kuna majadiliano ndani ya Serikali kuona hilo linafanyikaje. Tungojee hayo majadiliano ndani ya Serikali halafu yakifikia muafaka tunaweza tukajua ni nini kitakachofanyika. Kwa sababu hilo si suala la Wizara ya Afya pekee yake, hilo linahitaji masuala mengi kama vile utumishi, Wizara ya Katiba na mambo mengine.