Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jonas Van Zeeland

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mvomero

Primary Question

MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua migogoro ya Wakulima na Wafugaji Kata za Hembeti, Mkindo, Sungaji, Mtibwa, Kanga, Mziha na Doma?

Supplementary Question 1

MHE. JONAS V. ZEELAND: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kwanza nachukua nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake. Kwa kuwa Mvomero ni miongoni mwa Wiliya ambazo bado zina changamoto ya migogoro ya wakulima na wafugaji: Je, Serikali inamkakati gani wa kuendelea kuyafuta mashambapori yaliyopo Mvomero ili muweze kuwagawia wananchi na kupunguza tatizo hili la migogoro ya wakulima na wafugaji? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa Mvomero bado tuna migogoro ya ardhi pamoja na kwamba imepungua.

Je, Mheshimiwa Naibu Waziri yupo tayari kuongozana nami baada ya Bunge hili kwenda kutatua migogoro hii Mvomero? (Makofi)

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza yaliyoulizwa na Mheshimiwa Zeeland Mbunge wa Mvomero, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na jambo la mashamba, nataka kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali ilishakagua mashamba 75 na katika hayo, mashamba 15 yalishatolewa ilani ya kuendelea kufuatiliwa katika maana ya kufutwa au kuona utaratibu mwingine wowote, utakaofanyika. Katika hatua hizo, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba pale tutakapokuwa tumekamilisha taratibu nyingine zote tutamjulisha kwa niaba ya wananchi wake ili aweze kujua hatua Serikali ilizochukua.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la kuongozana mimi naye kwenda Jimboni kwa ajili ya kutatua migogoro hiyo, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba niko tayari baada ya hapa, kwa sababu ni njia ya kwenda Jimboni kwangu, nami nitasimama Mvomero pale tuweze kutengeneza mambo mazuri ili kuweka hali ya usalama na watu wetu wakae vizuri.