Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ng'wasi Damas Kamani

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NG'WASI D. KAMANI aliuliza: - Je, Serikali inatoa kauli gani kwa Makampuni Binafsi yanayouza Hisa na hayajatoa gawio miaka mingi pamoja na kujiendesha vizuri?

Supplementary Question 1

MHE. NG'WASI D. KAMANI: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, lakini bado jukumu la msingi la kulinda maslahi na vipato vya Watanzania linabaki kuwa la Serikali, basi swali langu la kwanza; je, Serikali inatambua uwepo wa makampuni haya ambayo Watanzania wamewekeza kwa kununua hisa yanafanya biashara, yanatengeneza faida na bado hayalipi magawio kwa Watanaznia hawa waliowekeza?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; Serikali inasemaje au ina mkakati gani wa kuja na mpango madhubuti na wa wazi wa kuhakikisha kwamba inalinda maslahi ya Watanzania hawa waliowekeza dhidi ya wizi huu wa kuaminiwa?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kamani, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza tumepokea shauri hilo na tunafuatilia mara moja. Nimwombe tu Mheshimiwa Mbunge tuwe na mashirikiano ya pamoja katika kuzitambua kampuni hizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, nielekeze DSE na CMA kufanya uchunguzi juu ya tuhuma hii ya wizi na mara tu zitakapobainika hatua za kisheria zitachukuliwa.

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. NG'WASI D. KAMANI aliuliza: - Je, Serikali inatoa kauli gani kwa Makampuni Binafsi yanayouza Hisa na hayajatoa gawio miaka mingi pamoja na kujiendesha vizuri?

Supplementary Question 2

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Nafahamu pamoja na kwamba sheria hiyo ipo na sisi ndio tunaosimamia utawala wa sheria, lakini nafikiri pia makampuni haya yanasimamiwa kwa regulation za taratibu zetu za nchi.

Sasa tunaomba kujua Serikali ina mpango gani sasa wa kuitisha taarifa za mashirika hayo ili kujua wametoa gawio kiasi gani na tangu walipoanza kuuza hisa wametoa gawio kiasi gani na kuwapa wananchi taarifa nini hatma yao?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jesca, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, hili ni shauri na shauri lake tumelichukua, tunaenda kulifanyia kazi.