Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa elimu kwa vijana walio mashuleni juu ya kujikinga na dawa za kulevya?

Supplementary Question 1

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

(a) Kwa kuwa vitendo vya kikatili vya kupiga wanafunzi vimekuwa vingi katika shule. Je, Wizara ya Elimu italiambia nini Bunge hili, usalama wa wanafunzi wanapokuwa shuleni?

(b) Kwa kuwa, walimu wanaofanya vitendo hivyo, wanaangaliwa wanapokuwa wanakwenda shuleni kwamba hawana viashiria vya ulevi hata wakafanya vitendo vya kikatili vya namna hiyo? (Makofi)

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Fakharia Shomar Khamis, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kwenye suala la Walimu na matendo yanayokithiri ya kupiga wanafunzi tayari Wizara ya Elimu imekwisha kuanza kuchukua hatua mahsusi za kufanya ufatiliaji kwenye maeneo yote ambayo tumekuwa tukipata taarifa kwamba wanafunzi wanatendewa visivyo, kinyume na utaratibu wa kisheria.

Mheshimiwa Naibu Spika, vivyo hivyo katika hatua nyingine kupitia Wizara yetu Ofisi ya Waziri Mkuu, tunaweza tukashirikiana vizuri na Wizara ya Elimu ili kuweza kubaini kama matendo hayo ya wale watuhumiwa ambao wanaonekana wametenda matendo ya ukatili kwa watoto, kama itaonekana kwamba wana viashiria vya ulevi basi tutachukua hatua kuweza kuhakikisha kwamba masuala haya hayajitokezi tena katika nchi yetu na kuchukua hatua zinazostahili. (Makofi)