Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE K.n.y. MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza: - Je, ni lini mgogoro wa mipaka kati ya Vijiji vya Utengule, Ovindembo, Ipinde, Tanganyika na Kampuni ya Kilombero North's utatatuliwa?

Supplementary Question 1

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Mheshimiwa Kunambi, swali lake hapa linauliza ni lini Serikali itatatua mgogoro huu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; ili kupunguza migogoro na kuimarisha sense of ownership kati ya Mlima Kilimanjaro na Vijiji vya Foo, Mkuu, Ndoo, Kilanya, Sawe, Ng’uni na kule Kieli, Serikali ilituahidi kutuletea fedha za CSR ili tujenge madarasa; nawe Mheshimiwa Naibu Waziri uliahidi hapa Bungeni kwamba mtatupa fedha hizo: Je, ni lini Serikali itatuletea fedha hizo za CSR? Ahsante.

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Saashisha kwa niaba ya Mheshimiwa Godwin Emmanuel Kunambi, Mbunge wa Mlimba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nifafanue kwenye suala la lini Serikali itatatua mgogoro? Kwenye jibu langu la msingi nimeeleza kwamba, kwa sasa hivi Kamati ya Mawaziri nane imeshapita maeneo takribani yote hapa nchini, na imeacha kila mkoa kamati inayofanya tathmini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna baadhi ya maeneo tayari uthamini umeshaanza, lakini kuna maeneo ambayo tayari wananchi walikuwa wameshavamia kwenye maeneo kama hilo la kilombero. Tunafanya tathmini kuangalia eneo lipi ambalo litakuwa ni la muhimu kuokoa kile kiini ambacho kitatunza haya maji kwa ajili ya kuyapeleka katika Bwawa la Mwalimu Nyerere.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tathmini hii iko uwandani inafanyika na inashirikisha wananchi wa Mlimba hatua kwa hatua ili kuangalia nini kilicho sahihi ili kusije kukaleta mkanganyiko tena kwamba kamati hii haikushirikisha wananchi. Kwa hiyo, ni lini? Ni pale ambapo tu kamati hii itakapokamilisha uthamini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye suala la CSR, naomba tu tena niendelee kuelekeza TANAPA; nakumbuka tulifanya ziara na Mheshimiwa Saashisha katika maeneo ya hai, lakini tukaangalia, kweli kulikuwa kuna uhitaji wa wananchi katika eneo hilo ambalo wanatakiwa wapate CSR.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nielekeze TANAPA tukamilishe ahadi hii kwa wananchi ili tuweze kuwa na ushirikiano mzuri na wananchi waweze kuwa ni sehemu ya uhifadhi kwa ajili ya kizazi cha sasa na cha baadaye, ahsante.

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE K.n.y. MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza: - Je, ni lini mgogoro wa mipaka kati ya Vijiji vya Utengule, Ovindembo, Ipinde, Tanganyika na Kampuni ya Kilombero North's utatatuliwa?

Supplementary Question 2

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nataka nimwulize Mheshimiwa Waziri kwamba ni lini Serikali itakuja kutatua mgogoro uliopo katika Halmashauri ya Ushetu pamoja na Kariwa ambao unazidi kuchukua sura mpya na sasa mpaka wananchi wangu zaidi ya 17 wamekamatwa na kuwekwa ndani bila sababu zozote za msingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nipate majibu ya Serikali.

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cherehani, Mbunge wa Ushetu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, nampa pole Mheshimiwa Mbunge, na pia nawaomba wananchi wa Ushetu wawe na subira. Tulipanga kwenda kufanya mazungumzo na wananchi, lakini ratiba zikaingiliana. Nawaomba wananchi wa Ushetu wawe wavumilivu, baada ya Bunge hili, tutaondoka na Mbunge wao kwenda kuzungumza na kutatua changamoto hii, ahsante. (Makofi)

Name

Regina Ndege Qwaray

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE K.n.y. MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza: - Je, ni lini mgogoro wa mipaka kati ya Vijiji vya Utengule, Ovindembo, Ipinde, Tanganyika na Kampuni ya Kilombero North's utatatuliwa?

Supplementary Question 3

MHE. REGINA N. QWARAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Kumekuwa na mgogoro wa muda mrefu kati ya Hifadhi ya Tarangire na Vijiji vya Olasiti, Kakoyi na Vilima Vitatu.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kumaliza kabisa ule mgogoro wa eneo hilo? (Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Regina, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali imejipanga kupunguza ama kumaliza kabisa migogoro iliyopo baina ya hifadhi zinazozunguka maeneo ya wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na hili nimuahidi kwamba kupitia Kamati ya Mawaziri nane lakini pia kwenye migogoro mipya inayokuja tumejipanga kuitatua bila kuleta taharuki kwa wananchi. Kwa hiyo, nitaenda na nitashirikiana na wataalam kuangalia wapi penye marekebisho na tutazungumza na wananchi tutaitatua hii changamoto.