Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara ya kuunganisha Ruaha Mbuyuni, Malolo hadi Uleling’ombe?

Supplementary Question 1

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa, barabara hii ya kutoka Ruaha Mbuyuni kupitia Malolo, Ibanda, Mlunga, Uleling’ombe, Kinusi mpaka Wilaya ya Mpwapwa ndiyo kiungo kati ya Mkoa wa Morogoro na Mkoa wa Dodoma, na kwa kuwa Kata ya Uleling’ombe ndiyo Kata ambayo kiuchumi inalisha maeneo mengi ya Jimbo la Mikumi pamoja na Wilaya ya Mpwapwa.

Je, Serikali haioni kwamba wakati umefika sasa wa kuiweka barabra hii katika vipaumbele vya kuunganisha Mkoa wa Morogoro na Mkoa wa Dodoma?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dennis Lazaro Londo, Mbunge wa Jimbo la Mikumi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa mwenyekiti, tumetambua umuhimu wa barabara hiyo na ndiyo maana umeona katika mwaka wa fedha unaokuja tumeitengea fedha, kwa sababu awali barabara hii ilikuwa haipo katika mtandao wetu. Kwa hiyo, nimthibitishie Mbunge wa Jimbo la Mikumi, barabara hiyo tutaitengea fedha na itajengwa kama mapendekezo ya Mbunge lakini kutokana na umuhimu wa kuunganisha Mkoa wa Morogoro na Dodoma. Ahsante sana.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara ya kuunganisha Ruaha Mbuyuni, Malolo hadi Uleling’ombe?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza.

Barabara ya Mahenge inayopita Udekwa inatokeza mpaka Ilula ni barabara muhimu sana, ni barabara mbadala ya barabara ya Mlima wa Kitonga kama magari yakikwama.

Je, ni lini Serikali itaipa umuhimu mkubwa sana ili barabra hii ijengwe kusiwepo na matatizo inapotokea katika barabra ya Kitonga, magari yaweze kupita katika hii barabra? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Ritta Kabati, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Iringa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabra ya Mahenge mpaka kwenda Ilula kama barabara ya mchepuko tunatambua umuhimu wake na tutawatuma TARURA Mkoa wa Iringa waende wakafanye tathmini halisi na watuletee ili tutafute fedha kwa ajili ya utengenezaji. Ahsante sana. (Makofi)