Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Rashid Abdallah Shangazi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mlalo
Primary Question
MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itasimamia kwa dhati sheria zake na kuondosha unyonyaji na ukandamizaji unaofanywa na wachuuzi kwa kununua mazao ya wakulima kwa utaratibu wa kufunga lumbesa?
Supplementary Question 1
MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri napenda kumfahamisha kwamba tunakwenda kwenye Tanzania ya viwanda na kule Mlalo tunalima kabichi, karoti, viazi, hoho pamoja na mazao mbalimbali ya mboga mboga. Je, haoni kwa kuwa sisi tutakosa viwanda wakatutafutia soko zuri la kuweza kupata tija kwenye mazao haya?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa mazao na bidhaa nyinginezo zinafungwa katika vipimo ambavyo vinaeleweka, haoni sasa ni wakati wa Serikali kuweka mkazo kwamba na mazao ya wakulima nayo yaweze kufungwa katika utaratibu ambao utawaletea tija wakulima? Ahsante.
Name
Charles John Mwijage
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Muleba Kaskazini
Answer
WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu soko la mazao, katika maelekezo ambayo Serikali imetoa na Mheshimiwa Waziri Mkuu katika hotuba yake amesisitiza ni kwamba Halmashauri zote kuanzia ngazi ya Kijiji, Kata mpaka Wilaya tunapaswa kutenga maeneo ambayo moja itakuwa sehemu ya kujenga viwanda vidogo, pili itakuwa sehemu ya kujenga hifadhi na tatu itakuwa sehemu ya kufanyia biashara. Kwa kutengeneza zile business centers, wateja wataweza kufika na kuweza kununua mazao yenu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mazao ya wakulima yakifungashwa vizuri yatapata soko, nakubaliana na hilo. Jambo la kufanya ni kwamba tunapohimiza ujengaji wa viwanda huko vijijini vinaongeza thamani na unapoongeza thamani ya bidhaa inahusisha pamoja na ufungaji. Kwa mfano, tungependa watu wa Lushoto na Tanga zile tangawizi na hiliki mkishazichakata kwenye viwanda vidogo pale ndiyo zinaingia kwenye packaging ambayo itakuwa inaeleza kama ni kilo au ni volume gani.
Mheshimiwa Shangazi tutawasiliana zaidi kusudi niweze kukupa maelekezo ya kiutendaji.
Name
Martha Moses Mlata
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itasimamia kwa dhati sheria zake na kuondosha unyonyaji na ukandamizaji unaofanywa na wachuuzi kwa kununua mazao ya wakulima kwa utaratibu wa kufunga lumbesa?
Supplementary Question 2
MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa tatizo la lumbesa linasababishwa na viroba ambavyo vina vipimo tofauti tofauti. Kwa kuwa nchi yetu ilikuwa na kiwanda cha magunia ambayo yalikuwa na kipimo na ujazo ulio sawasawa.
Je, Waziri yupo tayari kwenda kukifufua kiwanda kile ili tuweze kuwa na vipimo vinavyolingana kuepuka kuwadhulumu wananchi wetu? Ahsante.
Name
Charles John Mwijage
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Muleba Kaskazini
Answer
WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la viroba au vifungashio vyenye ukubwa tofauti suluhisho lake ni kuwa na mizani kwenye buying centre ambao utabainisha kilo stahiki, ukubwa wa gunia sio hoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la viwanda vya magunia, kwa nini viwanda vya mgunia vya Tanzania vilikufa ikiwemo kile cha Kilimanjaro. Magunia yanayotoka nchi za Asia ikiwemo Bangladesh yanapoingia East Africa hayatozwi ushuru, magunia yanayotengenezwa na viwanda vya Tanzania yanatozwa ushuru katika mazingira hayo lazima tuanguke. Kwa hiyo, mapendekezo ni kwamba lazima tuangalie ulinganisho wa ushuru na gharama za bidhaa zinazotoka nje na zinazoingia ndani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala hili limeshafikishwa kwa wahusika na tutaweza kulishughulikia namna hiyo. Kwa hiyo, viwanda vya Kilimanjaro, Singida na Tanzania nzima vitaweze kufufuka kwa namna hiyo.
Copyright © Bunge Polis 2024. All Rights Reserved