Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kurejesha Kambi ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Tunduru ili kuimarisha ulinzi?

Supplementary Question 1

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Swali la kwanza; kwa kuwa, Waziri amesema tayari mipango ya kufufua Kambi ile inaendelea na sasa hivi hali ya usalama upande wa kusini hasa upande wa Msumbiji sio nzuri katika Vijiji vya Wenje, Lukala, Nasomba, Makandi na Kazamoyo watu hawa wanaishi kwa kutokuwa na amani. Je, haoni sasa ni muhimu kuweka angalau makambi ya temporary ili kurejesha amani ya wananchi wa vijiji hivyo?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa vijiji hivyo kwa sasa ulinzi umekabidhiwa kwa mgambo ambao wako 30 katika vijiji hivyo na wanapewa sh.50,000/= kwa mwezi na Halmashauri.

Je, Serikali haioni sasa ni muhimu kuwalipa mshahara mgambo wale ili waweze kuendelea kulinda mipaka?

Name

Dr. Stergomena Lawrence Tax

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba nijibu maswali ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua hali ilivyo katika mipaka yetu yote ikiwa ni pamoja na mpaka wa Kusini na tayari hatua mbalimbali zimechukuliwa kuimarisha ulinzi, hatukai tu tukisubiri kambi. Kambi itakuja lakini hatua za kuimarisha ulinzi katika mipaka hiyo zinaendelea na ulinzi umeimarishwa.

Mheshimiwa Spika, swali la pili kuhusu malipo, kwa mgambo kuwa na mishahara upo utaratibu unaotumika kulipa Jeshi la Mgambo na utaratibu huo utaendelea kutumika. Ahsante.