Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO K.n.y. MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara ya kutoka Buza-Kilungule hadi Nzasa?

Supplementary Question 1

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa muda wa ujenzi wa barabara hii umekwisha, je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha barabara hii inaisha haraka ili kuondoa msongamano katika Barabara ya Kilwa?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, je, ni lini Serikali itamalizia kwa kiwango cha lami kipande cha kilometa tano cha Mbande- Kisewe mpaka Msongora?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Chaurembo Abdallah, Mbunge wa Mbagala, kwa pamoja, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza tutahakikisha kwamba barabara ile kipande ambacho kimebaki cha kilomita tano chote tunakijenga kwa kiwango cha lami ikiwa ni pamoja na kukamilisha daraja ambalo limeshakamilika na sasa tunachoendelea ni kuweka lami pale juu kwenye daraja ambalo tunalijenga.

Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kufikia mwakani barabara ile yote tutakuwa tumeijenga kwa kiwango cha lami ikiwa ni pamoja na kukamilisha hilo daraja ambalo lilikuwa ni changamoto kubwa sana kwa wananchi ambao wanatumia barabara hiyo.

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO K.n.y. MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara ya kutoka Buza-Kilungule hadi Nzasa?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Spika,
nakushukuru kwa kunipatia fursa ya kuuliza swali moja la nyongeza. Ujenzi wa barabara ya mwendokasi kwenda Mbagala pamoja na magari yanayotoka bandarini na kuingia bandarini na uwepo wa mizani katika eneo la bandari linaleta usumbufu mkubwa sana kwa wakazi wa Kigamboni ambao wanatumia Daraja la Nyerere. Je ni nini mkakati wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kuhakikisha kwamba adha wanazozipata wananchi zinaondokana na changamoto hizi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Faustine Ndugulile, Mbunge wa Kigamboni, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mkakati wa Serikali ni kuhakikisha kwamba barabara zote na hasa za mjini zinajengwa na kupanuliwa kwa maana ya magari yaweze kupita ama mawili ama matatu ama manne. Hata hivyo, kama kuna suala ambalo liko very specific kwa barabara ambayo ameainisha Mheshimiwa Mbunge, nitamwomba tuweze kuonana naye kama Wizara ili tuone kama kuna changamoto yoyote ambayo iko tofauti sana tuweze kuwa na mpango wa haraka kuweza kuondoa changamoto hiyo kwa hiyo barabara ambayo ameainisha Mheshimiwa Mbunge.

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO K.n.y. MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara ya kutoka Buza-Kilungule hadi Nzasa?

Supplementary Question 3

MHE. SAMWEL X. HHAYUMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Barabara ya Nangwa- Gisambalang-Kondoa inayotegemewa na Kata ya Gisambalang, Dirma, Simbai, Sirop na Wareta ina daraja ambalo limekatika toka mwaka 2019.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga hilo Daraja la Muguri B?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hhayuma, Mbunge wa Hanang, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, daraja alilolitaja ambalo liko sasa hivi kwenye usanifu na tunategemea kwenye mwaka wa fedha ujao daraja hilo lianze kujengwa. Ahsante.

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO K.n.y. MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara ya kutoka Buza-Kilungule hadi Nzasa?

Supplementary Question 4

MHE. MINZA S. MJIKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi hii. Napenda kuuliza swali moja.

Ni lini barabara ya kutoka Kolandoto mpaka Meatu itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Minza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Kolandoto kwenda Meatu ni kati ya barabara ambazo zimeainishwa kwenye Ilani, na pia zipo kwenye mpango wa kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami kuanzia na kilometa 92. Kwa hiyo, sasa hivi kinachosubiriwa ni Serikali kupata fedha ili ujenzi wa barabara hii uanze. Ahsante. (Makofi)

Name

Agnesta Lambert Kaiza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO K.n.y. MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara ya kutoka Buza-Kilungule hadi Nzasa?

Supplementary Question 5

MHE. AGNESTA L. KAIZA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Barabara ya kutoka Kinyerezi kupitia Segerea hadi Tabata Relini ni barabara ambayo imekuwa na changamoto kwa muda mrefu; na Serikali wamekuwa wakiahidi mara kwa mara bila ya utekelezaji.

Mheshimiwa Spika, napenda kufahamu kauli sahihi kuhusiana na barabara hii. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Lambert, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Segerea kwenda Relini niliijibu wiki iliyopita wakati Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Segerea alipoliuliza. Nilichosema na bado naendelea kusema, barabara ilikuwa imefumuliwa na kulikuwa na changamoto ya Mkandarasi. Tunapoongea sasa hivi, Mkandarasi yupo site kukamilisha vipande vyote ambavyo vilikuwa vimefumuliwa.

Mheshimiwa Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba hiyo barabara inaendelea kutengenezwa. Ahsante. (Makofi)

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO K.n.y. MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara ya kutoka Buza-Kilungule hadi Nzasa?

Supplementary Question 6

MHE. FLORENT L. KYOMBO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa nafasi hii. Kwa nyakati tofauti viongozi wetu wa kitaifa waliahidi wananchi wa Wilaya ya Misenyi kutengeneza barabara ya Mutukula kwenda Minziro, na kwa bahati nzuri Naibu Waziri alikwenda kutembelea eneo hilo, akapokelewa kwa shangwe, lakini mpaka leo barabara hii haijatengenezwa pamoja na kuingizwa kwenye bajeti.

Je, ni lini barabara hiyo ya Minziro - Mutukula itatengenezwa wananchi wapate huduma na kuinua shughuli za kiuchumi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kyombo, Mbunge wa Misenyi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli barabara hii nilitembelea. Ni barabara ambayo inafunguliwa upya. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa kuwa haikuwa kwenye mtandao, kwa hiyo, inaweza isionekane, lakini azma ya Serikali ni kuifungua na kuijenga hii barabara. Ahsante.

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO K.n.y. MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara ya kutoka Buza-Kilungule hadi Nzasa?

Supplementary Question 7

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Barabara ya Mgakorongo kwenda mpaka Mrongo ni barabara muhimu ya kiuchumi kwa Mkoa wa Kagera lakini pia inaunganisha nchi jirani ya Uganda. Barabara hii ni lini itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Bilakwate, Mbunge wa Kyerwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja ni barabara kuu inayounganisha Tanzania na Uganda kupitia mpaka wa Murongo ambayo inaanzia Umugakarongo - Kigarama hadi Murongo.

Mheshimiwa Spika, tunavyoongea sasa hivi, taratibu za manunuzi zinaendelea na ikiwezekana barabara hii itatangazwa kabla ya mwisho wa mwaka huu wa fedha.

Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO K.n.y. MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara ya kutoka Buza-Kilungule hadi Nzasa?

Supplementary Question 8

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Barabara ya Utegi – Kowaki – Kinesi ni barabara iliyoahidiwa na Mheshimiwa Dkt. John Joseph Pombe Magufuli toka akiwa Waziri wa Ujenzi. Nataka nijue ni lini sasa utekelezaji wa ujenzi wa lami wa barabara hii kutoka Kowaki mpaka Kinesi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Rorya kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii iliahidiwa na kiongozi. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali imeratibu ahadi zote ikiwepo na hii barabara ambayo ameianisha. Nimhakikishie kwamba barabara hii itajengwa kadri Serikali itakapopata fedha. Ahsante.

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO K.n.y. MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara ya kutoka Buza-Kilungule hadi Nzasa?

Supplementary Question 9

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona. Barabara ya Guguni inaanzia Tengeru Sokoni hadi Mererani, inaunganisha mikoa miwili ya Arusha na Manyara.

Je, ni lini Serikali itaanza kujenga barabara hii kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Pallangyo Mbunge wa Meru, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, bahati nzuri barabara hii naifahamu, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii ipo kwenye mpango wa kujenga kwa kiwango cha lami na tukizingatia inakwenda kwenye migodi yetu kule Tanzanite. Ahsante.