Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza: - Je, nini kinakwamisha ujenzi wa barabara ya Mnivata – Masasi kupitia Tandahimba na Newala?

Supplementary Question 1

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa hii. Barabara ya kilometa zaidi ya 300 ambayo inatoka Lumecha Kupitia Msindo – Mputa – Kitanda mpaka Londo kwa Mpepo Morogoro, imefanyiwa Upembuzi na usanifu wa kina kwa muda mrefu sana.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami kwa haraka sana.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jacqueline Msongozi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya inayoanzia Lumecha- Kilosa kwa Mpepo, Malinyi hadi Ifakara kama alivyoisema, tumejibu mara kwa mara kwamba imeingizwa kwenye mpango wa EPC+F, na hivi tunavyoongea wakandarasi wameshaoneshwa hizo barabara na wako wanaandaa zabuni kwa ajili ya kuijenga kwa mfumo huo wa EPC+F, ahsante.

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza: - Je, nini kinakwamisha ujenzi wa barabara ya Mnivata – Masasi kupitia Tandahimba na Newala?

Supplementary Question 2

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa majibu mazuri. Wananchi wangu wa Mitesa Namalenga, Mdibwa, Nagaga, Chungutwa pamoja na Mpeta, wote hawa wamekuwa wakitarajia ujenzi. Sasa, kwa niaba yao nauliza, ni lini ujenzi huu utaanza?

Mheshimiwa Spika, lakini pili, kuhusu fidia, nimemsikia amejibu kwamba fidia imeanza, namuomba Waziri anijibu kwa asilimia ngapi jibu hili lina ukweli? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Issa Ally Mchungahela, Mbunge wa Lindi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa vijiji vyote alivyovitaja kwamba barabara hii itajengwa. Tulishatangaza na tumesema tumefungua; na kwa kuwa inafadhiliwa na African Development Bank, mchakato wa manunuzi tuna uhakika by March barabara hii itaanza kujengwa, japo sisi tunasema tayari tumeshaanza kulipa fidia mchakato unaendelea.

Mheshimiwa Spika, lakini kwa swali lake la pili, kwa asilimia ngapi, nataka nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwenye jimbo lake, jumatatu watakuwa hapo wanalipa fidia kwani tayari Mnivata hadi Chikwaya Wilaya ya Mtwara tayari tumeshalipa, baada ya Tandahimba itakwenda Newala na Masasi na fedha ipo tayari, ahsante. (Makofi)

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza: - Je, nini kinakwamisha ujenzi wa barabara ya Mnivata – Masasi kupitia Tandahimba na Newala?

Supplementary Question 3

MHE: EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Spika, Serikali itaanza lini ujenzi wa kilometa 30 kwa kiwango cha changarawe kutoka Uyogo kupita Iberansua, Mbika mpaka Urowa, ambapo barabara hii imekuwa kiungo kikubwa sana kwa wananchi na uchumi wa halmashauri wa Ushetu na mpaka tunavyoongea sa hizi magari yanadondoka ya wakulima wanaosafirisha mazao yao?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Nyongeza la Mheshimwa Cherehani, Mbunge wa Ushetu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii kama alivyosema inahitaji kujengwa kwa changarawe. Sehemu ya barabara hii ilikuwa chini ya barabara ya TARURA na sasa ndo imepangiwa bajeti. Nataka nimuhakikishie

Mheshimiwa Mbunge kwamba mwaka huu tutakwenda kuikarabati barabara hiyo. Nitumie nafasi hii kumuagiza Meneja wa Mkoa wa Shinyanga aende aitembelee hii barabara na kuifanyia ukarabati wa haraka ili kuokoa maisha na mali na hayo magari ya wananchi. Ahsante.

Name

Shamsia Aziz Mtamba

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza: - Je, nini kinakwamisha ujenzi wa barabara ya Mnivata – Masasi kupitia Tandahimba na Newala?

Supplementary Question 4

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi ili niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Barabara ya uchumi inayoanzia Mtwara Mjini kuelekea Msimbazi kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shamsia Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara iliyoitajwa tayari tumeshaifanyia upembuzi wa kina, Serikali sasa inatafuta fedha kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza: - Je, nini kinakwamisha ujenzi wa barabara ya Mnivata – Masasi kupitia Tandahimba na Newala?

Supplementary Question 5

MHE. DKT.CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, kwenye barabara ya Himo kuelekea Rombo, eneo wanalovuka wanafunzi wa Shule ya Korona na maeneo yale yanayokaribia masoko ya Kisambo na Mwika ni hatari sana kwa wapita njia lakini kwa magari pia. Je, Serikali ipo tayari kujenga matuta kwenye maeneo hayo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Charles Kimei, Mbunge wa Vunjo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, suala la matuta ni suala ambalo linategemeana na wataalam. Naomba niwaagize wataalam wa TANROADS hasa Meneja wa Mkoa wa Kilimanjaro, aende akafanye usanifu ili aone kama kuna umuhimu wa kufanya suala hilo. Ni vyema akawasiliana na Mheshimiwa Mbunge ili aone maeneo ambayo anahitaji suala hili linakotakiwa kufanyika, ahsante.

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza: - Je, nini kinakwamisha ujenzi wa barabara ya Mnivata – Masasi kupitia Tandahimba na Newala?

Supplementary Question 6

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Barabara ya Mtoni - Bombo kwenda mpaka Bashewa, na barabara hiyo hiyo kutokea upande wa Maramba mpaka Tanga, usanifu wake lini utaanza? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dunstan Kitandula, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii ni barabara ambayo tumeitengea fedha kwa ajili ya kukamilisha usanifu wa kina mwaka huu wa fedha. Kwa hiyo, nina uhakika barabara hii mwaka huu itaanza kufanyiwa usanifu wa kina. Ahsante.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza: - Je, nini kinakwamisha ujenzi wa barabara ya Mnivata – Masasi kupitia Tandahimba na Newala?

Supplementary Question 7

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Ni nini kinakwamisha ujenzi wa barabara kipande cha Haydom mpaka Labay?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Flatei Massay, Mbunge wa Mbulu Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hakuna kinachokwamisha ujenzi wa barabara hii. Zabuni ya kwanza ilitangazwa kilometa 25 ambayo inatoka Mbulu Mjini hadi Galbad; na kuanzia Labay - Haydom, barabara hii zabuni za kuitangaza zinaendelea. Kwa hiyo, awe na Subira, zikikamilika taratibu za manunuzi, barabara hii itatangazwa kwa kilometa nyingine 25 lakini pia barabara hii imeingizwa kwenye EPC+F. Ahsante.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza: - Je, nini kinakwamisha ujenzi wa barabara ya Mnivata – Masasi kupitia Tandahimba na Newala?

Supplementary Question 8

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya Kinyanambo C - Mapanda hadi Kisusa katika Jimbo la Mufindi Kaskazini? Maana ilikuwa imeahidi kujenga kilometa tano tano na ni barabara ya kiuchumi.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Ritta Kabati, Mbunge wa Viti Maalum, Iringa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja itajengwa kwa kiwango cha lami kufuatana na upatikanaji wa bajeti. Kwa hiyo, Serikali itaendelea kutafuta fedha kuijenga kwa kiwango cha lami barabara hiyo. Ahsante.

Name

Mrisho Mashaka Gambo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arusha Mjini

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza: - Je, nini kinakwamisha ujenzi wa barabara ya Mnivata – Masasi kupitia Tandahimba na Newala?

Supplementary Question 9

MHE. MRISHO M. GAMBO: Mheshimiwa Spika, naomba kufahamu barabara ya kutoka uwanja mdogo wa Airport Arusha mpaka eneo la Kilombero kwa kiwango cha njia nne utaanza lini; na hasa ukizingatia kwamba barabara hii ikikamilika itasaidia kuondoa msongamano na changamoto ya mafuriko kwenye Kata za Ungalimitedi, Sombetini na Usunyai?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mrisho Gambo, Mbunge wa Arusha Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli barabara ya Airport kwenda Kilombero ni barabara ya muhimu kwenda njia nne; na ujenzi wa barabara hii kama ilivyo kwenye Majiji mengine utategemea sana upatikanaji wa fedha. Nadhani labda kwenye mpango huu tunaouendea, basi tutaomba tuweze kuanza kuweka mpango wa kuijenga barabara hii kwa kiwango cha barabara nne ili kupunguza msongamano katika Mji wa Arusha. Ahsante.