Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Khalifa Mohammed Issa

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Mtambwe

Primary Question

MHE. KHALIFA MOHAMED ISSA K.n.y. MHE. MOHAMED SAID ISSA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuhakikisha TBS na ZBS zinafanya kazi kwa ushirikiano?

Supplementary Question 1

MHE. KHALIFA MOHAMED ISSA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza, kwa niaba ya Mheshimiwa Mohamed Said Issa.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; je, utekelezaji wa makubaliano hayo umefikiwa kwa kiasi gani?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; je, Serikali ipo tayari leo kutoa tamko kuwa bidhaa zilizotambuliwa na moja katika mashirika mawili hayo hutumika nchi nzima bila ya utambuzi wa Shirika lingine lolote nchini? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Khalifa Issa Mohamed, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa makubaliano haya umeshaanza na unaendelea kama nilivyosema kwenye maeneo yale yote matano kwa maana viwango vile tunavyokubaliana vinatekelezwa, lakini pia na bidhaa zote zinatambuliwa katika pande zote mbili.

Mheshimiwa Spika, kwenye swali la pili, ndio hii moja ya vitu ambavyo tumesisitiza katika sehemu ya tano, kwamba lazima bidhaa zote ambazo zimethibitishwa na ZBS au na TBS kwa upande wa Bara zinatambuliwa katika pande zote mbili.

Mheshimiwa Spika, hii si kwa Tanzania tu ni kwa Jumuiya yetu ya Afrika Mashariki kwamba hata ukienda kwenye bidhaa ambazo zimetoka kwenye nchi hizi za Jumuiya ya Afrika Mashariki ambazo taasisi zao za udhibiti wa viwango zimethibitishwa, zikija huku kwetu zinatambuliwa. Kwa hiyo, si kwetu tu kwa maana ya Zanzibar na Tanzania Bara, lakini pia hata Jumuiya ya Afrika Mashariki. Nakushukuru sana.