Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga Chuo cha VETA Nyangh’wale?

Supplementary Question 1

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza. Kwanza naipongeze Serikali kwa uamuzi wake wa kujenga VETA katika wilaya 63 ikiwemo Nyangh’wale. Naomba niulize maswali mawili: La kwanza, ni kiasi gani cha fedha ambacho kimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa VETA katika Wilaya ya Nyangh’wale? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Ni lini ujenzi huo utaanza mara moja? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Amar, Mbunge wa Nyangh’wale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kiasi kilichotengwa kwa ajili ya ujenzi wa Chuo hiki katika awamu ya kwanza kwa sababu vyuo vitajengwa kwa awamu, tumetenga zaidi ya Shilingi bilioni 1.4 kwa ajili ya kuanza awamu ya kwanza ya ujenzi huu. Suala la lini; hivi sasa tayari Wizara imeshapeleka maombi kwa wenzetu wa Wizara ya Fedha, tunasubiri upatikanaji wa fedha hizo. Mara tu fedha hizo zitakapopatikana kutoka Wizara ya Fedha, basi huo ujenzi utaanza mara moja.

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga Chuo cha VETA Nyangh’wale?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Kwa kuwa Chuo cha VETA kinachojengwa pale Mhula Jimboni Ukerewe kipo kwenye hatua za mwisho kabisa za ukamilishaji, ni lini Chuo hiki kitaanza kutoa huduma? Nashukuru sana.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Napenda kujibu swali dogo la Mheshimiwa Mbunge wa Ukerewe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Serikali ilikuwa imeanza ujenzi wa vyuo 25 katika wilaya 25 pamoja vile vinne vya mikoa na ujenzi ule upo kwenye hatua za mwisho. Hivi sasa tuko katika ukamilishaji wa vifaa vya kufundishia pamoja na samani ambazo tutapeleka mle madarasani. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika mwaka ujao wa 2023 vyuo hivi 25 vya Wilaya na vile vinne vya mikoa vitaanza kutoa mafunzo rasmi.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga Chuo cha VETA Nyangh’wale?

Supplementary Question 3

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba nimwulize Mheshimiwa Naibu Waziri: Ni lini Wizara ya Elimu itasaidia kwa dharura ujenzi Kituo cha VETA kule Nyamwaga, Nyamungo, kwa sababu fedha zimeshatengwa tangu mwaka 2021 mpaka sasa hivi imekaa inasubiri tu usaidizi wa Wizara yake? Ahsante. (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyojibu katika swali langu la msingi kwamba ujenzi wa Vyuo vya VETA katika Wilaya 63 tunatarajia kuanza mara tu fedha zitakapopatikana na miongoni mwa maeneo yatakayofikiwa ni pamoja na wilaya yake. Kwa hiyo, nimwondoe wasiwasi, ujenzi huo utaanza mara tu fedha hizo zitakapopatikana. Nashukuru sana.

Name

Furaha Ntengo Matondo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga Chuo cha VETA Nyangh’wale?

Supplementary Question 4

MHE. FURAHA N. MATONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Ilemela hakuna Chuo cha VETA, lakini wameshaandaa eneo lenye ekari 70.

Je, ni lini Serikali itaanza kujenga Chuo cha VETA katika Wilaya ya Ilemela ili kuondoa changamoto kwa vijana wetu ya kukosa ajira? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBUWAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Mheshimiwa Mbunge anachosema kwamba Wilaya ya Ilemela haina Chuo cha VETA na ni kweli eneo tayari limeshatengwa na tayari tulishakabidhiwa eneo hilo rasmi sisi kama Wizara kupitia wenzetu wa Mamlaka ya VETA. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Wilaya hii ni miongoni mwa zile Wilaya 63 ambazo zitapata mgao huu wa fedha hizi awamu ya kwanza kwa ajili ya kuanza ujenzi katika eneo hilo la Ilemela. (Makofi)

Mhesimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. (Makofi)

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga Chuo cha VETA Nyangh’wale?

Supplementary Question 5

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa kuzingatia ushauri wa Mheshimiwa Waziri wa Elimu, tayari Kijiji cha Mpanga, Kata ya Kisawasawa, Halmashauri ya Mji wa Ifakara, Wilaya ya Kilombero, imepata eneo la ujenzi wa Chuo cha VETA.

Je ni lini ujenzi wa chuo hicho utaanza?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la Mheshimiwa Asenga, Mbunge wa Kilombero kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spiuka, kama nilivyojibu kwenye majibu yangu ya swali la msingi kwamba Wilaya ya Kilombero ni miongoni mwa Wilaya 63 ambazo zipo kwenye mpango huu wa ujenzi wa vyuo vya VETA. Nimwondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge, tunasubiri fedha kutoka Wizara ya Fedha. Mara tu fedha zitakapopatikana, basi Wilaya ya Kilombero ni miongoni mwa Wilaya 63 ambazo ujenzi utaanza rasmi.

Name

Hassan Zidadu Kungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga Chuo cha VETA Nyangh’wale?

Supplementary Question 6

MHE. HASSAN Z. KUNGU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Wilaya ya Tunduru ni kati ya Wilaya ambazo hazina vyuo vya VETA, na eneo la ujenzi wa Chuo tayari tumeshaliandaa na lipo: Je, ni lini Serikali itatujengea Chuo cha VETA katika Wilaya ya Tunduru? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali dogo la Mheshimiwa Hassan, Mbunge wa Tunduru, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyojibu kwenye jibu la msingi kwa wilaya zote 63, ujenzi utaanza mara moja mara tu tutakapopata fedha kutoka Wizara ya Fedha na Mipango. Ujenzi huo tunatarajia kuanza kwenye Wilaya zote kwa pamoja ikiwemo na Wilaya ya Tunduru. Nakushukuru sana.

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga Chuo cha VETA Nyangh’wale?

Supplementary Question 7

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa nia njema Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa ilikabidhi Chuo cha VETA pale Mikumi kwa Serikali; na tangu Serikali imekabidhiwa, hakuna ukarabati na Chuo kinaendelea kuchakaa.

Je, ni kanuni au sheria kutowekeza fedha za ukarabati katika vyuo ambavyo Serikali imepewa bure?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Londo, Mbunge wa Mikumi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tuna Chuo cha VETA pale Mikumi ambacho hakijafanyiwa ukarabati na majengo yake ni chakavu. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge katika mwaka huu wa fedha 2022/2023 tumetenga fedha kwa ajili ya ukarabati pamoja na upanuzi kwenye baadhi ya maeneo ambayo vyuo hivi bado havijakamilika au vina miundombinu ambayo ni chakavu pamoja na hiki Chuo cha Mikumi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga Chuo cha VETA Nyangh’wale?

Supplementary Question 8

MHE. NOAH L. MOLLEL: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi.

Je, ni lini Serikali itajenga VETA katika Halmashauri ya Wilaya ya Arusha katika Jimbo la Arumeru Magharibi ambayo tayari tumeshawasilisha eneo kwa ajili ya kujenga VETA?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la Mheshimiwa Mbunge wa Arumeru kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyoeleza kwenye majibu yangu ya msingi, wilaya 63 ambazo hazina Vyuo vya VETA tunatarajia kuanza ujenzi mara tu tutakapopata fedha ikiwemo na Wilaya ya Arumeru.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.