Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE auliza: - Je, Serikali ni lini italeta Bungeni Muswada wa Sheria ya Kampuni Binafsi za Ulinzi?

Supplementary Question 1

MHE. ATHUMAN A. MAIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Je, Serikali inakiri kuwa muda wa miaka sita tangu ichukue Muswada huu ni mrefu sana kutoletwa Bungeni?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, wakati tunajadili kupata maoni ya Muswada huu tuligundua kwamba kipengele kile cha kubeba silaha Upande wa Zanzibar kisingekubaliwa. Je, tukiongeza maneno “isipokuwa Zanzibar” katika kipengele kile kitafanya Muswada huu uamke na kuletwa Bungeni?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu mawali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Maige kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, uandaaji wa sheria, hasa hizi ambazo zinahitaji ushirikishwaji mpana wa jamii hususani kwenye hili ambalo linahusu pande mbili za Muungano ni jambo ambalo miaka sita huwezi ukasema ni muda mrefu sana. Ni muda mrefu lakini ili tupate sheria itakayokubalika kwa pande zote na wadau wote tunaomba Mheshimiwa atuvumilie tuweze kulikamilisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu maoni ya kubeba silaha upande wa Zanzibar kwamba kuna changamoto pengine hicho kipande kiondolewe, naomba Mheshimiwa asubiri michakato ya Baraza la Mapinduzi Zanzibar na Baraza la Mawaziri wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yaweze kukamilisha kazi yake tuweze kuwasilisha Muswada huo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.