Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUBIRA K. MGALU aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kugawa mashine za kutolea risiti EFD kwa Wafanyabiashara ili kuongeza wigo wa walipa kodi?

Supplementary Question 1

MHE. SUBIRA K. MGALU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwanza naishukuru sana Serikali kwa majibu mazuri na naipongeza TRA na wadau mbalimbali kwa ubunifu huo wa mashine ambayo inarahisisha, sasa maswali yangu mawili ya nyongeza ni kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa bado yapo matukio ambayo baadhi ya wafanya biashara ya kutotoa risiti hasa katika maeneo yenye biashara mfano Kariakoo. Je, Serikali kupitia TRA kwa kuwa imepewa kibali kwa mara ya kwanza kaujiri watumishi wengi kwa wakati mmoja, inawatumiaje watumishi wale katika mapambano dhidi ya vitendo hivi vya kutotoa risiti? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, kwa kuwa katika jibu lake la msingi ameeleza kwamba, wafanyabiashara wanaruhusiwa kusheria kurejesha gharama za mashine za EFD wanazozinunua wakati wanakokotoa mapato ya kutoza kodi. Je, Serikali inajipangaje kutoa elimu hii kwa wafanyabiashara wengi ili kuondoa dhana ya kwamba mashine za EFD ni gharama zaidi? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Subira Khamis Mgalu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote kabla ya kujibu maswali haya, kwa idhini yako, naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa namna anavyofuatilia na pia ni Balozi wa TRA.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la kwanza, Serikali iliwapatia mafunzo yale ambayo ni muhimu kabisa, awali kabla ya kuanza kufanya kazi, lakini kama hilo halitoshi, Serikali imeandaa Mkakati wa kutoa mafunzo ya watumishi hawa, mafunzo maalum kwa watumishi hawa wapya kila baada ya miezi minne.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, Serikali kupitia TRA ina program ya kutoa elimu kupitia vyombo vya habari, tv pamoja na redio. Nichukue fursa hii kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, kuwaelekeza TRA kuendelea kutoa mafunzo hayo kimkakati. Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUBIRA K. MGALU aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kugawa mashine za kutolea risiti EFD kwa Wafanyabiashara ili kuongeza wigo wa walipa kodi?

Supplementary Question 2

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuweza kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kuna kipindi kumekuwa kukitokea tatizo la upatikanaji mfumo hasa kwa watu wanaohitaji zile mashine za EFD, hivyo kuchelesha kupata zile mashine za EFD nini mkakati wa Serikali wa kuimarisha mfumo ili wafanyabiashara waweze kupata hizi mashine za EFD kwa wakati? Ahsante.

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Toufiq, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto hizo zilikuwepo za mfumo huo wa mashine ya EFD na ndiyo maana tukaamua sasa kuleta mfumo mpya na kifaa kipya ambacho kinajulikana kwa VFD. Ahsante. (Makofi)