Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuwapatia vifaa vya kisasa wananchi wanaofanya shughuli za kukausha dagaa?

Supplementary Question 1

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza na nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina swali moja la nyongeza. Kwa kuwa wanawake wengi ndiyo wanajishughulisha na ukaushaji wa dagaa, je, Serikali ina mpango gani maalum wa kuwasaidia kwa haraka wanawake hawa ili kupata tija zaidi? (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Maryam Mwinyi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mpango maalum tulionao, la kwanza Serikali imejikita katika kulitangaza zao la dagaa kuwa ni zao la kimkakati na lengo na dhamira ya Serikali ni kulipa thamani zao hili kulifungulia masoko na kuweza kuwahakikisha hata mabenki yaweze kuwa na utayari wa kuwakopesha akinamama wanaojishughulisha na shughuli hizi za ukaushaji wa dakaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili ni kufungua masoko ya duniani na hivi tunavyozungumza zao la dagaa limekuwa na thamani kubwa sana katika soko la dunia.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na hayo pia kama nilivyosema katika jibu la msingi ni kuwawezesha kupata mikopo kupitia Benki yetu ya kilimo na kuhimiza halmashauri zetu kupitia ile asilimia nne ya akinamama, kuwasaidia na kuwakopesha zaidi akinamama wazalishaji hasa kundi hili la wavuvi linalokausha dagaa na kufanya biashara hii ya dagaa. Ahsante.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuwapatia vifaa vya kisasa wananchi wanaofanya shughuli za kukausha dagaa?

Supplementary Question 2

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa hii. Kwa kuwa dagaa ni shughuli ambayo wanawake wanajishughulisha nayo sana na shughuli hii inaendana sambamba na suala zima la mwani. Je, Serikali ina mpango gani kuhusiana na suala la mwani kuwasaidia wanamwani hawa kutupatia vifaa? Sambamba na vifaa kutupatia au kututafutia soko la mwani kwa ajili ya ustawi wa wanawake?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Salma Kikwete, Mbunge wa Mchinga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mkakati wetu katika mwani, kwenye bajeti yetu ya mwaka huu wa fedha 2022/2023, tumetenga takribani Shilingi Bilioni 3.4 kwa ajili ya kununua vifaa kwa maana ya kamba, taitai na mbegu kwa ajili ya kuzitawanya katika vikundi vya akinamama mwambao wote wa pwani kuanzia Mkinga mpaka kule Moa Mtwara.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini vilevile mkakati wetu ni kujenga maghala, nia ni madhumuni ni kuongeza uzalishaji. Hivi sasa tunazalisha tani 3,500 tunataka tufike tani 10,000 hadi 15,000 ili sasa tuwe na kauli katika soko.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba tu nimhakikishie Mheshimwia Salma Kikwete lakini na Wabunge wote kwamba, Serikali tumejipanga vema, tunalo lengo hata la kuingiza mwani katika mtindo wa stakabadhi ghalani ili tuweze ku-control bei ambayo kwa muda mrefu sana imeonekana ni yenye kuyumba. Ahsante sana.

Name

Mwantumu Mzamili Zodo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuwapatia vifaa vya kisasa wananchi wanaofanya shughuli za kukausha dagaa?

Supplementary Question 3

MHE. MWANTUMU M. ZODO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa kuwa Serikali katika bajeti yake ya mwaka 2021/2022 ilituahidi vichanja kwa wavuvi wa dagaa; na kwa kuwa hata kwenye bajeti yake ya 2022/2023, bado ametuahidi vichanja na Mheshimiwa Naibu Waziri amesema kuna vichanja 80 watapeleka. Je, ni lini sasa Serikali itapeleka vichanja hivyo? (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swal la nyongeza la Mheshimiwa Zodo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niseme kabisa mwaka huu niliousema wa fedha wa 2023/2024, baada ya kuwa tumekamilisha taratibu zote za kitaalam, ambazo ndiyo zilizokuwa zikitukwamisha tutakwenda kutekeleza ahadi hii ya Serikali kwa hakika kabisa.

Name

Dr. Alice Karungi Kaijage

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuwapatia vifaa vya kisasa wananchi wanaofanya shughuli za kukausha dagaa?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Nami naipongeza Serikali kwa kuja na mradi mzuri huu wa kuinua wavuvi na kwa kuwa Wilaya za Mkuranga na Kibiti ni wilaya ambazo zinajihusisha na uvuvi sana na kundi kubwa la wanawake wanafanya shughuli hii. Je, ni lini mradi huu wa kuinua wavuvi utawafiki wananchi wa wilaya hizi mbili? Ahsante.

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalum, Mheshimiwa Dkt. Alice Kaijage, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Mkuranga na Kibiti ni miongoni mwa wilaya zitakazofaidika na program hii, lakini vilevile zitafaidika na program kubwa inayokwenda kwa jina la Tanzania Scaling up Blue Economy ambapo tutajenga maghala ya kuhifadhia samaki, masoko vikiwemo na hivi vichanja. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Dkt. Alice na Wabunge wengine wa Mkoa wa Pwani, Tanga, Lindi na Mtwara pamoja na wengine wote kwamba tumejipanga vema na hili tunakwenda kutekeleza.