Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua migogoro ya mikataba ya minara ya simu kati ya kampuni za simu na Kijiji cha Namuchinka Kata ya Kapele?

Supplementary Question 1

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Spika, ahsante.

Mheshimiwa Spika, nimepokea majibu ya Serikali na ninamshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa ufafanuzi. Swali langu la kwanza lipo katika mfumo wa ombi, je, Naibu Waziri anaonaje kama atatafuta siku ya weekend katikati ya Bunge hili la Bajeti aongozane nami kwenda Jimboni Momba, kunisaidia kutoa ufafanuzi kwa wananchi wa Kijiji cha Namchinga ili waweze kuelewa?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, je, Serikali inaonaje kama itatoa mwongozo kwa makampuni haya ya simu ili kuhakikisha wanapolipa pango la ardhi kwa Mmiliki lakini watoe na percent kwenye Serikali ya Mamlaka husika, aidha, Serikali ya Mtaa au Kijiji ili kutoa mgongano wa maslahi kwenye jamii.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Condester Michael Sichalwe, Mbunge wa Momba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa kazi kubwa anayoifanya. Siku mbili tatu hizi tumekuwa tukiongea na Wenyeviti wa Vijiji, Wenyeviti wa Mtaa na Mwenyekiti wa Kata katika Kijiji hiki cha Namchinga. Kwa kweli anafanya kazi kubwa sana na hakika Jimbo la Momba wamepata Mbunge kwelikweli.

Mheshimiwa Spika, vilevile kuhusu suala la kwenda kutoa elimu, naomba nilipokee na tutakaa tutajadili kadri nafasi itakavyoweza kupatikana tutaweza kufanya hivyo. Nakuhakikishia Mheshimiwa Mbunge tutafanya kulinganana na nafasi itakayopatikana.

Mheshimiwa Spika, jambo jingine kuhusu suala la kutoa percent kwa wananchi wetu na dhana kubwa ambayo inasababisha kwamba wananchi wanahitaji kupewa percent kuna dhana imejengeka kwamba minara hii iliyopo katika maeneo ya wananchi ina mionzi ambayo inawaathiri sana wananchi kiasi kwamba wanataka hii percent kama fidia.

Mheshimiwa Spika, Wabunge na wananchi wote, nikuhakikishie kwamba minara hii kiwango ambacho kimewekwa katika minara yetu, kiwango cha chini ni Volt Saba per meter, lakini minara yetu nchi nzima iko chini ya Volt Saba maana yake ipo kati ya Tatu mpaka Nne. Kwa hiyo, suala la mionzi naomba huu mtazamo tuutolee elimu ya kutosha ili wananchi wafahamu.

Mheshimiwa Spika, vilevile kwa Sheria ya Mwaka 2009, iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2020 inasema kabisa kwamba makampuni ya simu yatatoa asilimia 0.3 kwenye Halmashauri kulingana na minara inayotumika katika Halmashauri husika. Ahsante. (Makofi)