Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Igawa hadi Tunduma kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. SUMA I. FYANDOMO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pia nashukuru kwa majibu ya Serikali kwamba imejiandaa kwa ajili ya kuanza ujenzi wa bypass, hata hivyo nina maswali ya nyonge. La kwanza, je, ni lini wananchi ambao wanakaa Uyole mpaka Ifisi watalipwa fidia zao ili kupisha ujenzi wa barabara hiyo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, naomba kwa uzito wake, kuanzia Uyole mpaka Mbeya Mjini mpaka kufika airport ile barabara haina hata service road kwa maana hiyo mabasi, bajaji, maguta, malori pamoja na ambulance ambazo zinapeleka wagonjwa wa rufaa Mbeya, lakini usiombe kama unakwenda airport unaweza ukapaki gari pembeni ukapanda bajaji ama bodaboda ili kuwahi kule inakuwa shughuli.

Je, ni lini Serikali itatafuta Mkandarasi kwa haraka ili kuweza kuepusha ajali zinazotokea mara kwa mara kwa ufinyu wa barabara?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Suma Ikenda Fyandomo, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mbeya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nianze na suala la fidia kabla ya kuanza ujenzi wa barabara hii, fidia italipwa kwa wananchi ambao watapisha ujenzi huu. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Jiji la Mbeya kwamba Serikali italipa fidia kabla ya kuanza ujenzi wa barabara hii.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge lakini pia na Mheshimiwa Spika ambaye najua hili jiji ni jiji lako kwamba, ni kweli barabara hii ambayo Serikali imeamua kuchukua hatua za haraka sana kulingana na ukweli kwamba msongamano ni mkubwa.

Mheshimiwa Spika, tunatambua kwamba hatuna barabara hizi za kupaki bajaji na pikipiki lakini pia tunatambua kwamba barabara hii ndio inayopitisha mizigo karibu asilimia zaidi ya 50 ya mizigo inayotoka Bandari ya Dar es Salaam kwenda DRC, Zambia na Malawi na ndio maana Serikali imechukua jitihada na hatua za haraka kuhakikisha kwamba barabara hii inapanuliwa na wakati inafanya design ni pamoja na kutengeneza hayo maeneo ambayo yatakuwa ni ya kupaki malori, mabasi na bajaji.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kazi hii itafanyika na tayari tupo kwenye hatua za manunuzi ili tunavyoanza tu Julai kazi ianze ya ujenzi huu pamoja na hizo parking ambazo Mheshimiwa Mbunge amezisema. Kwa hiyo naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge hivyo. Ahsante sana. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, siku ya Jumanne liliulizwa swali la nyongeza la kuhusu hii barabara na majibu yako yalisema, ujenzi unaanza mwaka huu wa fedha ambao ni 2021/2022, majibu ya msingi hapa yanaonesha kwamba katika mwaka wa fedha 2022/2023, Sasa kwa sababu hapa umenitaja nimeona uliweke vizuri hilo tuwe tunajua 2021/2022 au 2022/2023. (Makofi)

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba niliweke vizuri suala hili. Kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi, tutaanza ujenzi kwa maana ya kupeleka mkandarasi site mara tunapoanza mwezi Julai, utekelezaji wa bajeti.

Mheshimiwa Spika, lakini kwenye jibu la msingi tunasema taratibu za manunuzi zimeshaanza kwa maana ya kutafuta Mkandarasi, kusaini zabuni na kuanza kufanya tathmini. Kwa hiyo, ujenzi tunasema tayari tumeshaanza kwa sababu hizo hatua zimeanza na kwamba tutakapoanza tu mwaka mpya Mkandarasi anakuwa yupo site. Lakini taratibu za manunuzi zimeshaanza na tayari tumeshatangaza. (Makofi)

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Igawa hadi Tunduma kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa barabara ya Kona ya Kiseriani ambayo inaungana na barabara ya Arusha bypass imekuwa kero kubwa sana na kusababisha msongamano wa magari katika Jiji la Arusha. Tumeona Mkandarasi amepatikana na muda wa kujiandaa umekwisha.

Je, ni lini sasa mkandarasi ataanza kazi ya kujenga barabara hii katika Jiji la Arusha?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Catherine Magige Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara zote za bypass lakini barabara zote za Mji wa Arusha, ziko kwenye mpango wa kujengwa. Kwa hiyo, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ziko kwenye taratibu mbalimbali za manunuzi ikiwa ni pamoja na barabara ya Arusha kwenda Kisongo, Arusha kwenda Usa River, lakini pia na barabara ambayo inaunganisha barabara ya Bypass ya Arusha Kusini ambayo inaunganisha Tengeru kwenda Usa River. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba taratibu zinaendelea za kuzijenga hizo barabara. Ahsante. (Makofi)

Name

Shabani Hamisi Taletale

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Igawa hadi Tunduma kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Spika, naomba kuuliza Serikali ni lini itaanza kujenga barabara yetu ya Bigwa
– Kisaki?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Taletale Mbunge wa Morogoro Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Bigwa – Kisaki ni kati ya barabara 22 ambazo ziko kwenye taratibu mbalimbali za manunuzi ili ujenzi wa barabara hii muhimu ya kutoka Bigwa – Kisaki, kwenda Bwawa la Nyerere uanze. Kwa hiyo, muda wowote taratibu zikikamilika, barabara hii itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami. (Makofi)

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Igawa hadi Tunduma kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. DANIEL B. SILLO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali moja. Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Babati, Galapo hadi Orkesumet kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Daniel Sillo, Mbunge wa Babati Vijiji, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii ni barabara muhimu ambayo tayari imeshakamilishwa kufanyiwa usanifu wa kina na Serikali inaendelea kutafuta fedha ili barabara hii ianze kujengwa kwa kiwango cha lami. Kwa hiyo, mara Serikali itakapopata fedha, barabara hii itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami, ahsante. (Makofi)

Name

Mariam Madalu Nyoka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Igawa hadi Tunduma kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. MARIAM M. NYOKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru.

Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Majengo, Ruvuma, Subira kwenda Mpitimbi kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mariam Nyoka, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Ruvuma, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kufanya kazi ya usanifu wa kina ili ianze kujengwa kwa kiwango cha lami.