Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO aliuliza: - Je, kuna Wataalam wangapi wa huduma za utengamano na mazoezi ya viungo physiotherapist katika Mkoa wa Morogoro?

Supplementary Question 1

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, umbali wa kutoka Morogoro Mjini mpaka Mikumi ni kilometa 120 na kutoka Mikumi mpaka Iringa ni kilometa 190, kuna ajali nyingi sana ambazo zinatokea katika kipande hiki na wanategemea sana huduma katika Kituo cha Afya na Hospitali hii ya Mtakatifu Kizito pale Mikumi.

(a) Je, Serikali haioni umuhimu wa kupeleka watalaam wa huduma wa utengamao na physiotherapy pale Mikumi? (Makofi)

(b) Je, Serikali haioni wakati umefika sasa kuokoa maisha ya Watanzania wengi kuanzisha centre of excellence ya wataalam wa mifupa kwa ajili ya kujifunza pale Mikumi? Naomba kuwasilisha. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maswali yake mawili moja la kuongeza watalaam. Moja, kwenye eneo la kuongeza watalaam suala tu siyo kuongeza watalaam lakini ni kushirikiana na wenzetu wa Wizara ya Mambo ya Ndani, lakini uchukuzi kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tunapunguza mambo ambayo yanapelekea ajali zitokee kwenye maeneo hayo, pia kuhamasisha elimu ya magonjwa yasiyoambukiza ili kupunguza idadi ya watu hao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubaliana na yeye kwamba Mkoa wa Morogoro ukiangalia wanahitajika watalaam 30 na kwa mwaka huu wanaenda kuongezwa watalaam tisa maana yake katika hawa tisa tutaona ni namna gani tunaweza kuhakikisha tunaongeza watalaam kwenye eneo ambalo yeye amelitaja. Lakini kuangalia vizuri zaidi data zilizotumika kuamua wanahitajika Mkoa wa Morogoro hawa 30 kuangalia kama ilitumika data za wakati gani ili kama kunahitajika kuongeza basi tuwaongeze.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine la wataalam wa mifupa na vitu vingine tunaenda kufikiria kwenye ajira ambazo amesema Mheshimiwa Waziri wa Utumishi ni 32,000 basi tutaenda kulizingatia eneo hilo wakati tukipata hivyo vibali. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Joseph Anania Tadayo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO aliuliza: - Je, kuna Wataalam wangapi wa huduma za utengamano na mazoezi ya viungo physiotherapist katika Mkoa wa Morogoro?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH A. TADAYO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kupata nafasi hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa huduma ya utengemao na mazoezi ya viungo ni muhimu sana kwa wagonjwa wanaopata matatizo yanayohusika na viungo, na kwakuwa Wilaya nzima ya Mwanga kuanzia Hospitali ya Wilaya mpaka vituo vyake vya afya hatuna matalaam hata mmoja wa huduma hiyo.

Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya kutupatia physiotherapist katika Wilaya ya Mwanga hasa ukizingatia ahadi ya Mheshimiwa Waziri wa Utumishi juu ya ajira lukuki zinazokuja kwa ajili ya afya. Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kuwapigania wananchi wa Mwanga, lakini yeye mwenyewe anajua sasa Rais wetu amepeleka fedha pale Mwanga kwa ajili ya kujenga Idara ya Dharura na ujenzi unaendelea. Wakati ujenzi unakamilika na kuweka vifaa na ajira 32,000 ambazo zimetokea hayo mambo yatakwenda kuzingatiwa kuhakikisha tunapomaliza huduma ya magonjwa ya dharura na watalaam wa aina hiyo uliowasema wanakuwepo vilevile kwenye eneo hilo. (Makofi)

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO aliuliza: - Je, kuna Wataalam wangapi wa huduma za utengamano na mazoezi ya viungo physiotherapist katika Mkoa wa Morogoro?

Supplementary Question 3

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru, hospitali ya Mji wa Tarime inahudumia zaidi ya wananchi wa Wilaya tatu na imekuwa ina uhaba wa watumishi wa afya wakiwemo watalaam wa utengamao na mazoezi ya viungo.

Je, ni lini sasa Serikali itatuletea watalaam hawa wa utengemao na mazoezi ya viungo? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa swali lake zuri, lakini nitamuomba Mheshimiwa Mbunge mimi na yeye tutashirikiana kuangalia kwa maana ya data za Wilaya hiyo na sehemu hizo, kwanza kwasababu amesema hospitali inatumiwa na Wilaya tatu, tutaangalia kuona tatizo lipo wapi.

Moja; kama kuna maeneo ambayo inaweza ikafanyika kwenye Wilaya husika wapelekwe kwenye Wilaya husika, lakini kwenye ajira ambazo zinakwenda kutokea tutaenda kuzingatia kwa kuangalia data za eneo husika na utumishi watakapotuletea kibali hayo yatazingatiwa. (Makofi)

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO aliuliza: - Je, kuna Wataalam wangapi wa huduma za utengamano na mazoezi ya viungo physiotherapist katika Mkoa wa Morogoro?

Supplementary Question 4

MHE. JUDITH S. KAPINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga siyo tu kwamba haina Daktari hata mmoja wa masuala ya viungo, lakini haina Daktari hata mmoja wa macho, meno na radiojia na anesthesia.

Je, Serikali inatuahidi nini katika kupata watalaamu hawa.

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Mbunge nampongeza sana jinsi ambavyo amekuwa na mchango mzuri sana hasa kwenye eneo la lishe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuambie majibu ni yale yale kwamba kwenye ajira 32,000 pia tutachukua kwa kushirikiana na yeye lakini tutawauliza watalaam wa eneo husika kwa kuangalia load ya wagonjwa wanaohitaji huduma ya mtengamao kwenye eneo alilolitaja ili tuweze kuamua mapema na kupeleka mahitaji Utumishi ili kuweza kupata hao watalaamu ambao Mheshimiwa anawataja.

Name

Tabasamu Hamisi Hussein Mwagao

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sengerema

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO aliuliza: - Je, kuna Wataalam wangapi wa huduma za utengamano na mazoezi ya viungo physiotherapist katika Mkoa wa Morogoro?

Supplementary Question 5

MHE. TABASAM H. MWAGAO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Naomba kuuliza swali la nyongeza kwa Mheshimiwa Naibu Waziri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Naibu Waziri ulikuja Sengerema nikaalika mkutano mkubwa sana na ukaahidi katika kituo cha Busisi kukipa vifaa, leo mwaka unakwisha unaniandalia kitu gani huko Jimboni kwangu. Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimjibu Kaka yangu Mheshimiwa Tabasam ni kweli nimekwenda kwenye eneo husika, tulifanya pamoja naye mkutano wa wananchi na tuliahidi mbele ya wananchi, nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa kushirikiana na wenzangu wa TAMISEMI, tayari Kituo cha Afya cha Busisi kipo kwenye maombi ya dharura ambayo sasa yanaenda kutekelezwa mwaka huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tayari imeshaingizwa kwenye mpango na fedha zinaenda kupelekwa kwa ajili ya kufanya kazi tuliyokubaliana siku ile kwenye mkutano. (Makofi)