Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara kuu ya Mwanza - Shinyanga kwa kiwango cha njia nne kutoka Mwanza Mjini hadi Usagara?

Supplementary Question 1

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya swali la nyongeza. Naomba nimwulize Mheshimiwa Waziri, kwani barabara hii ni muhimu sana kwa wananchi wa Jimbo la Nyamagana na Jiji la Mwanza kwa ujumla, ukizingatia kwa sasa tuna mradi mkubwa wa daraja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pamoja na upembuzi yakinifu unaokamilika mwezi huu, naomba Mheshimiwa Waziri anihakikishie kwamba baada ya upembezi yakinifu kukamilika na bajeti itakuwa imeshaanza, kwenye mapitio ya bajeti, Serikali itakuwa tayari kuhakikisha barabara hii inaingia kwenye mpango na kuanza kujengwa upya?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mabula, Mbunge wa Nyamagana kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba mwezi huu wa Nne tarehe 27 tutakamilisha usanifu wa kina. Kama alivyoomba kwamba baada ya kukamilika Serikali itafanya nini kwenye mid review ya bajeti ya Wizara?

Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, Serikali imesikia ombi lake, nasi tunajua msongamano wa barabara hiyo. Tumelichukua na tutaangalia jinsi ya kufanya pale itakapokamilika na kujua gharama ya barabara hii. Ahsante. (Makofi)

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara kuu ya Mwanza - Shinyanga kwa kiwango cha njia nne kutoka Mwanza Mjini hadi Usagara?

Supplementary Question 2

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. barabara Kolandoto - Munze - Mwangungo yenye kilometa 63 ni barabara ambayo imo katika mpango wa Ilani ya Utekelezaji ya Chama cha Mapinduzi na pia ipo katika mpango wa bajeti ya 2021/2022: Ni lini utekelezaji wa mradi huu utaanza kutekelezwa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli barabara Kolandoto - Mwangungo kwenda Lalago ni barabara ambayo iko kwenye ilani na imekuwa ikipangiwa bajeti. Barabara hii ni ndefu inayokwenda mpaka Sibiti - Mbulu, kwa maana ya Hyadom – Mbulu. Barabara hii imeanza kutekelezwa kwa vipande na kwa sasa tutaanza ujenzi wa kipande cha Mbulu – Hyadom kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara kuu ya Mwanza - Shinyanga kwa kiwango cha njia nne kutoka Mwanza Mjini hadi Usagara?

Supplementary Question 3

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Mheshimiwa Waziri Mkuu mwaka 2020, wakati anafunga kampeni za uchaguzi katika Jimbo la Ushetu, alipokea simu kutoka kwa aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt. Magufuli na akawaahidi maelefu ya wananchi pale kwamba atawajengea kilometa 54 za lami kutoka Kahama – Nyandekwa - Iboja mpaka Iyogo kilometa 54 za lami: je, ahadi hii itaanza kutekelezwa lini kwa wananchi wa Ushetu? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Ushetu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo tumekuwa tukisema, ahadi zote za viongozi wa Kitaifa ni ahadi ambazo zinatekelezwa. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara zote ambazo zimeahidiwa tunazo lakini tunaendelea kuzitekeleza kadri ya upatikanaji wa fedha ikiwa ni pamoja na hii barabara ambayo Mheshimiwa Rais aliahidi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii pia itajengwa kwa kiwango cha lami kama ambavyo Mheshimiwa Rais aliagiza. Ahsante. (Makofi)

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara kuu ya Mwanza - Shinyanga kwa kiwango cha njia nne kutoka Mwanza Mjini hadi Usagara?

Supplementary Question 4

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Ipo dhamira ya Serikali ya kuunganisha mikoa yote kwa barabara za lami. Mkoa wa Singida ni miongoni ni mwa mikoa ambayo haijaunganishwa na mikoa mingine ukiwemo Mkoa wa Simiyu na Mkoa wa Mbeya.

Je, dhamira ya Serikali ya kujenga barabara ya Mkiwa – Itigi – Rungwa hadi Makongorosi imefikia wapi kuanza kujengwa? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Massare, Mbunge wa Itigi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii ni barabara kuu ambayo inatoka Mkiwa – Itigi - Rungwa hadi Makongorosi – Chunya. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii ni kati ya barabara 22 ambazo ziko kwenye maandalizi ya kuanza kujengwa kwa kiwango cha lami kuanzia Mkiwa kwenda Manyoni mwaka huu wa fedha kilometa 50. Ahsante.

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara kuu ya Mwanza - Shinyanga kwa kiwango cha njia nne kutoka Mwanza Mjini hadi Usagara?

Supplementary Question 5

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Barabara ya kutoka Newala kuelekea Masasi kupitia Mitesa imechukua muda mrefu sana kuanza licha ya kwamba fedha ipo, kwa nini barabara hii imechukua muda mrefu kiasi hiki? Lini barabara hii itaanza kujengwa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mchungahela, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nimemsikia vizuri, anaongelea barabara ya Newala kwenda Masasi kuanzia Munivata. Barabara hii ilishapatiwa fedha na ipo kwenye maandalizi ya kuanza ujenzi wa kiwango cha lami. Kwa hiyo, suala tu ni kwamba, mikataba tayari inaandaliwa kwa ajili ya kuanza kujenga barabara hii kwa kiwango cha lami kuanzia Mnivata, Newala hadi Masasi yenye urefu wa kilometa 160 kama nimemwelewa vizuri.

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara kuu ya Mwanza - Shinyanga kwa kiwango cha njia nne kutoka Mwanza Mjini hadi Usagara?

Supplementary Question 6

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Nami napenda kujua ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha njia nne barabara kuu ya TANZAM, kipande cha Uyole mpaka Songwe kupitia Mbeya Jiji na Mbalizi? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Njeza, Mbunge wa Mbeya Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Jiji la Mbeya ni kati ya majiji ambayo yana changamoto kubwa sana ya usafiri katika kipindi hiki; na Serikali ina njia mbili ya kutatua changamoto hizi. Moja, ni kujenga bypass ya kuanzia Uyole hadi Songwe yenye urefu wa kilomita 49; na pia kupanua barabara inayopita katikati kutoka njia mbili kwenda njia nne.

Mheshimiwa Spika, hatua ya haraka ambayo Serikali imechukua ni kupanua kwanza njia mbili kwenda njia nne kuanzia Uyole hadi Songwe eneo la Ifisi kilomita 29 na taratibu za manunuzi zinaendelea hadi tunavyoongea hapa sasa kwa mwaka huu wa fedha. Ahsante. (Makofi)

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara kuu ya Mwanza - Shinyanga kwa kiwango cha njia nne kutoka Mwanza Mjini hadi Usagara?

Supplementary Question 7

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kuniona. Kwa kuwa kuwa barabara kuu ya Makambako – Songea inayopitia katika Mji wa Njombe imezidiwa na inahitaji ukarabati mkubwa: Je, ni lini barabara hii sasa itaanza kukarabatiwa au kujengwa upya? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Deodatus Mwanyika, Mbunge wa Njombe Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba barabara aliyoitaja ambayo inaanza Makambako, Njombe hadi Songea ni kati ya barabara za zamani sana kujengwa miaka ya 1984. Tayari usanifu ulishakamilika na Serikali inaongea na Word Bank ili tuweze kupata fedha kwa ajili ya kuikarabati barabara hii. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali tayari ipo kwenye mchakato wa kuongea na hizi taasisi za kibenki kwa maana ya kifedha ili tukishafanikiwa basi ukarabati wa barabara hii uanze.

Name

Philipo Augustino Mulugo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songwe

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara kuu ya Mwanza - Shinyanga kwa kiwango cha njia nne kutoka Mwanza Mjini hadi Usagara?

Supplementary Question 8

MHE. PHILLIPO A. MULUGO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Ujenzi wa barabara ya lami kutoka Mbalizi mpaka Mkwajuni, upembuzi yakinifu na usanifu umekamilika na mwaka huu wa fedha Mheshimiwa Naibu Waziri wa Fedha, aliniahidi kwamba mwaka 2022/2023 watatenga fedha kwa ajili ya kukamilisha barabara hiyo lami. Je, anakumbuka; na kwamba tayari mwaka huu wameshatenga fedha za barabara hiyo? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mulugo, Mbunge wa Songwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba ni dhamira ya Serikali kujenga barabara zote kwa kiwango cha lami na hasa zile zinazounganisha mikoa na mikoa, wilaya na wilaya lakini pia barabara kuu na barabara muhimu. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba dhamira ya Serikali bado iko pale pale. Isipokuwa barabara ipi inaanza, inategemea kimsingi na bajeti ama na fedha itakayokuwa imepatikana kuanza ujenzi.

Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, dhamira Serikali bado iko pale pale kujenga barabara hizi kwa kiwango cha lami ikiwa ni pamoja na barabara ya Mheshimiwa Mulugo ambayo ameisema. Ahsante. (Makofi)

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara kuu ya Mwanza - Shinyanga kwa kiwango cha njia nne kutoka Mwanza Mjini hadi Usagara?

Supplementary Question 9

MHE. JERRY W. SILAA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kuniona. Naomba kuuliza swali dogo la nyongeza. Barabara ya Airport – Banana, Gongolamboto – Pugu - Chanika ndiyo barabara pekee kwenye Mkoa wa Dar es Salaam ambayo siyo double road. Naomba kujua mpango wa Serikali wa kuipanua barabara hii na kuwa ya njia nne.

Mheshimiwa Spika, ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jerry Silaa, Mbunge wa Ukonga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja ya kuazia Airport kwenda Gongolamboto ni sehemu ya barabara ya Nyerere Road. Barabara hii kama nimemwelewa Mheshimiwa Mbunge, ni barabara ambayo ipo kwenye awamu ya tatu ya hizi barabara za kwenda kwa kasi kwa maana ya BRT. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mkataba umeshasainiwa tarehe 17 Machi na Mkandarasi atakayejenga pale ni Sinohydro.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tunategemea muda wowote kuanzia pale katikati ya mji kwenda Gongolamboto barabara hii itaanza kujengwa kwa maana ya kupunguza msongamano kwa wananchi wa Dar es Salaam, hasa kwenye Jimbo la Mheshimiwa Silaa, Ukonga. Ahsante.

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara kuu ya Mwanza - Shinyanga kwa kiwango cha njia nne kutoka Mwanza Mjini hadi Usagara?

Supplementary Question 10

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Katika mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali ilitenga shilingi trilioni 1.5 kwenye Wizara ya Ujenzi na Bunge likapitisha. Mpaka Machi, mwaka huu 2022, imepewa asilimia 68 ambayo ni shilingi trilioni 1.09, hakuna barabara mpya hata moja iliyojengwa katika kipindi hiki cha mwaka fedha, sana sana wamelipa madeni: -

Mheshimiwa Spika, swali langu kwa Serikali, kwanini msiwe wakweli kwa Wabunge hawa, mkawaeleza kwamba mwaka huu tunalipa madeni, na mwaka ujao tunajenga barabara, kuliko kuwapa majibu mazuri ya matumaini wakati fedha hazipo? (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, kwanza nampongeza Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri aliyoyatoa; na niwahakikishie Wabunge pamoja na Watanzania kwamba fedha za kutekeleza hii miradi zipo; na Serikali inajenga barabara mpya na inalipa madeni. Ujenzi ule unavyofanyika, utaratibu wake ni kwamba kazi inapokamilika ndipo mtu analipwa. Tunalipa kwa certificate, hatugawi tu fedha zikasubiri mtu aanze kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa maana hiyo, kinachofanyika, tunatekeleza mradi, ukishakamilika tunalipa; na tunaendelea na miradi mipya, na yenyewe kadri certificate zinavyokuja tunalipa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hiyo anayosema ya madeni inawezekana kwenye hatua nyingine madeni yakawepo, kwa sababu ni lazima tufanye uhakiki; na miradi mingine ilishafanyika katika vipindi tofauti tofauti, kwa hiyo tuna uhakiki na tunalipa.

Mheshimiwa Spika, hivi ni kweli kwamba tungeweza kujenga reli inayokwenda mpaka Pacific, inayokwenda mpaka Bara lingine, inayokwenda mpaka upande mwingine wa bahari, halafu tushindwe kujenga barabara? (Makofi/ Kicheko)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge wote, tunajenga barabara mpya, tunalipa kwa certificate zinapokuwa tayari, lakini pia tunalipa na madeni ambayo kazi hizo zilishafanyika.

Mheshimiwa Spika, hatuwezi tukaacha kutengeneza barabara mpya wala kutekeleza miradi mipya tukafanya kazi moja ya kulipa madeni. Tutalipa madeni na tutatekeleza miradi mipya ya maendeleo.

Mheshimiwa Spika, haya ndiyo maelekezo ya Mheshimiwa Rais na hii ndiyo dira ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan. (Makofi)

Name

Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara kuu ya Mwanza - Shinyanga kwa kiwango cha njia nne kutoka Mwanza Mjini hadi Usagara?

Supplementary Question 11

MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Barabara ya Tegeta – Bagamoyo imejengwa na TANROADS na kuna sehemu ambayo hawajaweka mitaro kabisa, inasababisha mafuriko katika maeneo ya Basihaya na Tegeta: -

Mheshimiwa Spika, ni nini tamko la Wizara juu ya ku-repair eneo hilo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Kawe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, suala aliloliongelea la kusababisha mafuriko kwa sababu ya ujenzi wake kwa sababu ya barabara zimeinuka, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tumelichukua na ninaomba kutumia nafasi hii nimwagize Meneja wa Barabara wa Dar es Salaam aende akafanye study ya nini Wizara tufanye ili tuweze kuondoa changamoto hii kwa wananchi. Ahsante.

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara kuu ya Mwanza - Shinyanga kwa kiwango cha njia nne kutoka Mwanza Mjini hadi Usagara?

Supplementary Question 12

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi hii. Naomba kumwuliza Mheshimiwa Naibu Waziri, ni lini sasa Serikali itaanza ujenzi wa kiwango cha lami barabara inayotoka Kahama - Geita? Naomba Mheshimiwa Naibu Waziri anipe majibu ya kweli, barabara hii imekuwa ni kero ya muda mrefu.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Iddi Kassim Iddi, Mbunge wa Msalala, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Kahama – Ilogi kwenda Geita ni barabara ambayo inauganisha mikoa miwili; Mkoa wa Shinyanga na Mkoa wa Geita kupitia kwenye Jimbo la Mheshimiwa Iddi ambao ni Jimbo la Msalala.

Mheshimiwa Spika, ni kweli hii ni barabara ya kiuchumi na Serikali tumefanya majadiliano na wenzetu wa Barrick, lakini imeonekana bado wanasitasita kuanza kujenga hii barabara.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii sasa Serikali itaichukua ili ione namna ya kuifanya na pengine katika bajeti tunayoendelea kuiendea pengine tutaona nini cha kufanya ili tuanze kuijenga kwa kiwango cha lami.

Name

Munde Abdallah Tambwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara kuu ya Mwanza - Shinyanga kwa kiwango cha njia nne kutoka Mwanza Mjini hadi Usagara?

Supplementary Question 13

MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa fursa hii niulize swali la nyongeza. Barabara ya Tabora – Ulyankulu imekuwa sasa ni muda mrefu zaidi ya takribani miaka kumi imejengwa kilometa mbili tu za lami. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri ana mkakati gani sasa wa kuhakikisha barabara hiyo ya muda mrefu inakwisha? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge Munde, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba tu nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa kuwa Serikali imeshaonyesha nia na kama nilivyosema kwenye baadhi ya majibu yangu kwamba dhamira ya Serikali ni kuzijenga hizi barabara na tumeshaanza, lakini kuikamilisha barabara hii kwa kweli lazima tuseme itategemea na upatikanaji wa fedha. Pale fedha itakapopatikana basi Mheshimiwa Mbunge hii barabara tutaikamilisha kwa kiwango cha lami kama tulivyoahidi na kama tulivyoanza kujenga hizo kilometa za awali. Ahsante.