Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zuena Athumani Bushiri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kununua magari ya Polisi kwa ajili ya vituo vya Polisi nchini?

Supplementary Question 1

MHE. ZUENA A. BUSHIRI: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwanza nimshukuru Waziri kwa majibu mazuri ambayo ameyatoa, nina swali moja tu la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Mkoa wa Kilimanjaro ni mojawapo ya Mikoa ambayo ina uhitaji wa magari ya polisi hasa magari ya doria; je, Serikali ina mpango gani Mkoa wa Kilimanjaro kupata magari katika awamu hii ya kwanza ya magari 78 ambayo yanaingia nchini mwezi Aprili? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zuena Athumani Bushiri kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kutokana na jitihada zake anazochukua za kuhangaikia Mkoa wake wa Kilimanjaro basi tumepokea mapendekezo yake na tutahakikisha kwamba magari haya yakija tutaangalia uwezekano vilevile tuweze kupeleka Mkoa wa Kilimanjaro. (Makofi)

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kununua magari ya Polisi kwa ajili ya vituo vya Polisi nchini?

Supplementary Question 2

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru.

Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia kwamba Mkoa wa Songwe ni mpya na upo mpakani na kwenye jibu la Mheshimiwa Waziri amesema kwamba magari yatapelekwa kwenye maeneo ambayo yanauhitaji mkubwa, Mkoa wa Songwe una uhitaji mkubwa wa magari ya Polisi.

Mheshimiwa Spika, naomba kufahamu nini ahadi ya Serikali katika kuhakikisha kwamba tunatatua changamoto ya magari katika Mkoa wa Songwe? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Juliana Shonza, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Songwe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimejibu katika swali la msingi kwamba magari yale yatakapokuja tutayapeleka katika Mikoa ambayo ina uhitaji zaidi na Mheshimiwa Mbunge amethibitisha kwamba Mkoa wa Songwe ni moja kati ya Mikoa ambayo ina mahitaji basi tutalizingatia hilo.

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kununua magari ya Polisi kwa ajili ya vituo vya Polisi nchini?

Supplementary Question 3

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa hii nafasi.

Mheshimiwa Spika, swali langu ni kwamba hali ni mbaya katika Wilaya ya Mbozi hivi ninavyoongea Mkuu wa Polisi wa Wilaya hana gari hata la kutembelea. Kwa hiyo, katika hayo magari 78 Mheshimiwa Waziri naomba unihakikishie gari moja liende katika Wilaya ya Mbozi ili kumuokoa yule Mkuu wa Polisi wa Wilaya. Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nitakuwa sijakosea nadhani Wilaya yake ndiyo ile ya Mheshimiwa Silinde, kama hivi ndivyo hivi karibuni tulipeleka gari huko ambalo halikuwa jipya, kwa hiyo litasaidia nadhani tatizo litakuwa limepata ufumbuzi kama itakuwa siyo Wilaya hiyo ni Wilaya nyingine basi tutalizingatia vilevile. (Kicheko)

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kununua magari ya Polisi kwa ajili ya vituo vya Polisi nchini?

Supplementary Question 4

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa na mimi nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Liwale ilikuwa na gari moja tu ambalo kwenye Uchaguzi uliopita gari lile lilichomwa moto mpaka sasa hivi Wilaya nzima ile haina gari hata moja. Ni nini mpango wa Serikali kutupatia miongoni mwa hayo magari 78?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kwanza nikushukuru kwa kuliweka vizuri.

Mheshimiwa Spika, naomba nijibu sasa swali la Mheshimiwa Kuchauka Mbunge wa Liwale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimejibu kwenye swali la msingi kwamba magari haya yatakapokuja tutayapeleka katika maeneo ambayo yana mahitaji zaidi, kwa kweli maeneo ambayo yana mahitaji zaidi ni mengi kwa hiyo siyo rahisi kuweza kukamilisha kwa wakati mmoja kwa mwezi huu.

Kwa hiyo, niombe nikubaliane na Mheshimiwa Spika kwamba hoja za Waheshimiwa Wabunge tunajua ni za msingi, lakini magari yatakuja kwa awamu basi tutazingatia wapi kuna mahitaji zaidi.

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimejibu katika maswali yaliyopita ikiwemo na Mheshimiwa Mbunge Kuchauka kama itaangukia katika maeneo ambayo yana mahitaji zaidi na zaidi utapata mapema lakini nikuhakikishe kwamba tunafahamu na tunafanyia kazi. (Makofi)

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kununua magari ya Polisi kwa ajili ya vituo vya Polisi nchini?

Supplementary Question 5

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana swali langu dogo tu la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, pamoja na magari mengi ambayo mmeyatuma yatakuja kwa awamu. Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kutenga fedha za kutengeneza magari yaliyopo ambayo ni mengi tunayaona yapo katika vituo vingi vya Polisi ni mabovu. Sasa ni wakati mzuri labda muweze kutenga fedha ili tuweze kutengeneza haya yaliyopo tukisubiri hayo mageni, nashukuru. (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kilave Mbunge wa Temeke kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hoja yake ni ya msingi lakini nimhakikishie kwamba tumekuwa tukifanya hivyo na hata ndani ya Jeshi la Polisi tuna kitengo maalum kwa ajili ya matengenezo ya magari ya Polisi yale ambayo yanaweza kutengenezeka tunafanya hivyo na tutaendelea kufanya hivyo.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo tunafikiria kuja na mpango mwingine ambao utasaidia sana kuweza kutatua changamoto ya ubovu wa magari, nadhani wakati tutakapokuja kuwasilisha bajeti yetu hapa tutakuwa na nafasi pana zaidi ya kuweza kufafanua, lakini nimpongeze kwa wazo lake ni zuri na tunaendelea kulifanyia kazi na tutazidi kuliboresha zaidi.

Name

Tabasamu Hamisi Hussein Mwagao

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sengerema

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kununua magari ya Polisi kwa ajili ya vituo vya Polisi nchini?

Supplementary Question 6

MHE. TABASAM H. MWAGAO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Mheshimiwa Waziri ni kwamba hali ya gari la Sengerema anajua mpaka Mheshimiwa Simbachawene aliniahidi mwaka jana tutapata gari jipya. Sasa haya magari yanayokuja mwezi huu unanihakikishia gari moja linakwenda Sengerema kwa sababu hali iliyopo ni mbaya. (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa
Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Tabasam Mbunge wa Sengerema kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama mwongozo wako ulivyoutoa na kama ambavyo nimejibu nyuma kwamba tutapeleka magari haya kulingana na uhitaji zaidi, kwa hiyo tutaangalia kama Jimbo la Sengerema limeangukia katika eneo hilo atapata kama itabidi asubiri basi atapata siku za mbele pale ambapo yatapatikana magari ya ziada.

Name

Hassan Zidadu Kungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kununua magari ya Polisi kwa ajili ya vituo vya Polisi nchini?

Supplementary Question 7

MHE. HASSAN Z. KUNGU: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Tunduru ni Wilaya ambayo ipo mpakani na jiografia yake ni mbaya lakini pia kituo cha polisi kuna gari moja tu na tuna kilomita za mraba 18,778.

Je, Mheshimiwa Waziri anaweza kunihakikishia kwamba katika magari hayo 78 nasi tutapata gari moja? (Makofi/Kicheko)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba nirejee tena majibu yangu kama ambavyo nimejibu mwanzo kwamba tunatambua kwamba Jimbo la Tunduru lina uhitaji wa gari basi na lenyewe vilevile tumepokea.