Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ghati Zephania Chomete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GHATI Z. CHOMETE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuimarisha huduma za afya zikiwemo dawa muhimu katika hospitali zetu?

Supplementary Question 1

MHE. GHATI Z. CHOMETE: Mheshimiwa nakushukuru sana lakini pia nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, nina maswali madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kumekuwa na changamoto kubwa sana ya vifaa tiba ikiwemo vitanda vya kujifungulia akina mama katika Mkoa wa Mara.

Je, Serikali inawahakikishiaje wananchi na akina mama wa Mkoa wa Mara kwamba endapo italeta vifaa tiba hivyo hospitali pamoja na Vituo vya Afya vya Mkoa wa Mara vitapata vitanda kwa ajili ya kuondoa tatizo hilo?

Swali la pili; je, Serikali imejipanga vipi kuthibiti wizi wa dawa nchini?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa sababu siyo mara ya kwanza kufika Wizarani akizungumzia Hospitali yake ya Mkoa wa Mara. Lakini nimuondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge kwa sababu yeye anajua kwa sasa tayari vifaa vyenye thamani ya bilioni tatu zimeshapelekwa Mkoa wa Mara na hapa tunapoongea tayari CT Scan ipo pale Mkoani Mara na Digital Xray inangojea tu jengo liishe ili kazi ianze.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie kuwa hospitali ya Mkoa wa Mara tumeshakubaliana ndani ya Wizara na Waziri wa Afya ameshatoa maelekezo tarehe 12 na Mkoa wamekubaliana na maelekezo ya tarehe 12 Disemba hospitali hiyo inaenda kuanza na watumishi watahama kwenye hospitali waliokuwepo ili wahamie kwenye hospitali ya Mkoa.

Mheshimiwa Spika, lakini swali lake la pili la suala kuwa tumejipangaje kudhibiti wizi wa dawa. Moja, tumetengeneza mfumo ambao MSD sasa wataweza ku- track dawa kuanzia zinapotoka Taifani mpaka zinapofika kituoni. Wakati huo huo kama Wabunge mnakumbuka tulikuja hapa kwenu na kuwaonesha mianya ambayo inapotea dawa zinapofika kwenye Wilaya zetu na Mikoa yetu. Ushirikishwaji huo sio kwamba tulikuwa tunasema wizi wa dawa, lakini tulitaka kumleta kila mtu on board tujue wote ili tuweze kushirikiana kusimamia na sasa kule kwenye zahanati zetu, vituo vyetu vya afya, hospitali zetu za Wilaya tunashirikisha jamii na Waziri wa Afya ameshatoa maelekezo kwamba dawa ikitoka MSD inapofika Wilayani, Mkuu wa Wilaya ajue, Mkurugenzi ajue, lakini Mbunge apewe copy ili wote pamoja na zile Kamati za Afya za zahanati, za vituo vya afya na Wilaya wajue dawa iliyoingia ili kwa pamoja tushirikiane kulinda huu ubadhirifu ambao umekuwa ukitokea kwenye nchi yetu.

Name

Vedastus Mathayo Manyinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Mjini

Primary Question

MHE. GHATI Z. CHOMETE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuimarisha huduma za afya zikiwemo dawa muhimu katika hospitali zetu?

Supplementary Question 2

MHE. VEDASTUS M. MATHAYO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Kwa kuwa pale Musoma Mjini hatuna Hospitali ya Wilaya na nimekuwa nikiomba mara nyingi Serikali iweze kutukabidhi ile hospitali iliyopo ambayo ni ya Mkoa na imeahidi kwa muda mrefu.

Napenda kujua ni lini sasa rasmi Serikali itatukabidhi ile hospitali iwe Hospitali ya Manispaa ya Musoma ili huduma bora zaidi ziweze kupatikana kwa watu wetu?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kama ambavyo nimesema ni tarehe 12 Disemba, 2022 wanaanza kuhama kwenda kwenye hospitali mpya halafu mnakabidhiwa Hospitali ya Wilaya na ibaki kutumika namna hiyo.

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. GHATI Z. CHOMETE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuimarisha huduma za afya zikiwemo dawa muhimu katika hospitali zetu?

Supplementary Question 3

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tabora ya Kitete bado ina upungufu mkubwa wa dawa, je, Serikali imejipangaje kuhakikisha inapunguza tatizo hilo la upungufu wa dawa katika Hospitali ya Kitete?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kwa sababu kwa asilimia na kwa rekodi ambazo zimetoka MSD kwa sasa upatikanaji wa dawa ni asilimia 78 maana yake tuna upungufu wa asilimia 22. Moja ya namna ya kufanya ni kuchukua mapato ya ndani ambayo Hospitali ya Kitete inapata itumie kununua dawa palepale Tabora kama hazitakuwepo pale MSD.

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. GHATI Z. CHOMETE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuimarisha huduma za afya zikiwemo dawa muhimu katika hospitali zetu?

Supplementary Question 4

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, ahsante, Hospitali ya Kanda ya Mtwara bado inaupungufu mkubwa katika kuikamilisha kiujenzi, lakini pia vifaa tiba. Lakini Kanda yote ya Kusini inaitegemea hospitali hiyo kwa muda mrefu.

Sasa ni lini hospitali hiyo itakamilika ili kuwaondolea adha wananchi wa Kusini? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, kwanza niseme kwamba kwa kweli Hospitali ile ya Kanda ya Mtwara ni mojawapo ya hospitali nchini ambayo imejengwa kwa majengo ya kisasa mno. Lakini nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, pamoja na kazi kubwa ambayo imefanyika pale, mwaka huu wametengewa shilingi bilioni tano kwa ajili ya kuendelea na ujenzi ili kukamilisha mambo ambayo Mheshimiwa Mbunge anasema hayajakamilika. Niendelee kumpongeza Mheshimiwa Mbunge, kwa namna anavyofatilia shughuli za Mkoa wake.