Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA K.n.y. MHE. KABULA E. SHITOBELO aliuliza: - Je, ni sheria gani inayotumika kwenye tozo za bandari nchini?

Supplementary Question 1

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, pamoja na majibu mazuri ya Serikali ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Je Serikali haioni umuhimu wa kuwaelimisha watumiaji wa bandari ikiwemo ya Kemondo na Mwanza juu ya Sheria za Tozo zinazo zinazotungwa kuliko kukutana nazo barabani? (Makofi)

Swali langu la pili je, ni aina gani za tozo? Napenda kujua hilo, ahsante. (Makofi)

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Oliver Daniel Semuguruka, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, utaratibu wa kutoza tozo ama kutunga Sheria za Tozo kwanza unaanzishwa na Mamlaka ya Bandari yenyewe TPA na hatimaye unapelekwa kwa mdhibiti ambaye ndiye TASAC na TASAC ana wajibu wa kuitisha wadau wote wa sekta hiyo ama maeneo ambako hiyo tozo itakuwa inagusa katika tozo.

Sasa ninamuelekeza ambaye ndiye Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari nchini pamoja na TASAC watoe elimu, waende katika hizi bandari za Kemondo pamoja na bandari zingine nchini kwenda kutoa elimu kwa jamii ili waeleze ni aina gani ya tozo wakienda bandarini watakutana nazo na kwa kiwango gani.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili anataka Mheshimiwa Mbunge afahamu aina ya tozo ambazo bandari inatoza; tuna tozo ya aina nyingi, lakini zimegawanyika katika makundi mbalimbali; kuna tozo za lazima ambazo tunaita ni ports statutory charges, lakini kuna tozo tunazoziita wharfage, wharfage ni aina ya tozo ambayo ukitumia miundombinu ya bandari unatozwa, lakini kuna tozo za show handling hizi ni tozo ambazo meli inapokuja mpaka kwenye gati la bandari inapokuwa inashusha mzigo ama kupakia mzigo pia unatoza na kuna tozo za ziada, ahsante.

Name

Bahati Keneth Ndingo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA K.n.y. MHE. KABULA E. SHITOBELO aliuliza: - Je, ni sheria gani inayotumika kwenye tozo za bandari nchini?

Supplementary Question 2

MHE. BAHATI K. NDINGO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru; ni lini Serikali itaweza kupitia upya tozo hizi ambazo zimekuwa nyingi bandarini na kuleta uwekezaji kutochochewa kuhusiana na hizi tozo? Ahsante.

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Bahati Ndingo, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tunauchukua ushauri wa Mheshimiwa Mbunge na kimsingi tumeshaanza kukaa na wadau na mamlaka ambazo zinahusika kwa maana ya Tanzania ni TASAC, lakini kwa wenzetu Zanzibar ni ZMA ambako zina mahusiano ya moja kwa moja na vikao hivyo vinaendelea, na wewe Mheshimiwa Mbunge ukipata nafasi tutakukaribisha kama mdau ili utoe maoni ya Waheshimiwa wengine, ahsante.