Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Asya Sharif Omar

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASYA SHARIF OMAR aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua changamoto ya usafiri katika Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba?

Supplementary Question 1

MHE. ASYA SHARIF OMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza na kwanza naomba nimshukuru Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri. Lakini nataka kuuliza, je, kuna mkakati gani mahususi la kuongeza suala hili la usafiri katika Makao Makuu ya Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba, kwa sababu bado changamoto ni kubwa na hasa ukizingatia na vituo vidogo ambavyo vina mahitaji makubwa ya usafiri ikiwemo Kituo cha Mchangamdogo, lakini pia Kituo cha Mapana Kifuani ambacho nimekuzungumzia juzi? Ahsante sana.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Asya Sharif Omar kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema kwenye jibu la msingi, hivi sasa wamegaiwa magari matatu, tutaendelea kuwapatia magari ili wamudu kutekeleza majukumu ya ulinzi, usalama wa raia mali zao kadri tutakavyopata bajeti na kama anavyofahamu Mheshimiwa mwaka huu tumepitishiwa bajeti ya shilingi bilioni 15, yakanunuliwa magari, miongoni mwa maeneo yatakayopata magari ni pamoja na mikoa ya Pemba. Nashukuru.

Name

Khalifa Mohammed Issa

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Mtambwe

Primary Question

MHE. ASYA SHARIF OMAR aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua changamoto ya usafiri katika Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba?

Supplementary Question 2

MHE. KHALIFA MOHAMED ISSA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba nimuulize swali la nyongeza Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Spika, Zanzibar kuna polisi jamii, na polisi jamii hawa wanapelekwa kila Shehia katika Shehia za Zanzibar na shida yao kubwa ni mafuta.

Je, Serikali inatuambiaje kuwapatia walau mafuta, japo hawakupatiwa pikipiki lakini au maufta yakuwafikisha katika vituo vyao vya kazi? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Khalifa Mohamed Issa, Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli sio Zanzibar tu maeneo mbalimbali nchini Tanzania tunao utaratibu wa kuwa na polisi jamii kwa ajili ya kusaidia ulinzi shirikishi pale ambapo polisi wetu wanakuwa mbali na kwa sababu kama inavyoitwa polisi jamii uendeshaji wake kwa muda imekuwa ukichangiwa na wan jamii wenyewe. Sasa suala hili la kuzingatia kwenye upande wa mafuta ni suala kibajeti, tutalitafakari pale hali ya fedha na bajeti itakavyoruhusu tutaanza kuona uwezekano wa kuwafikiria mafuta na vyombo vya usafiri kama alivyotaja pikipiki. Nashukuru.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. ASYA SHARIF OMAR aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua changamoto ya usafiri katika Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba?

Supplementary Question 3

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Wilaya ya Nyang’hwale ina vijiji 62 kata 15 na OCD wetu pale Wilayani ana gari moja na si zuri sana; je, Wizara ina mpango gani wa kutuongezea gari nyingine polisi Nyang’hwale?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Amar, Mbunge wa Nyang’hwale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama alivyosema angalau yeye analo gari haliko vizuri sana lakini at least linatumika. Ushauri wetu gari hilo liendelee kukarabatiwa, lakini kama nilivyokwishasema wakati namjibu Mheshimiwa Asya, tunao utaratibu wa kununua magari na kuyapeleka kule ambako yanahitaji sana.

Kwa hiyo, Nyang’hwale, kama sehemu ya Mkoa wa Geita tutauangalia kulingana na upatikanaji wa hayo magari ili waweze kupata gari linawezesha OCD wetu kufanya kazi yake vizuri. Nashukuru.

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. ASYA SHARIF OMAR aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua changamoto ya usafiri katika Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba?

Supplementary Question 4

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Kishapu ina jumla ya kata 29 na ina vijiji 128 na Wilaya hii sasa haina gari hata moja, magari yote ni mabovu na kwa sasa hivi tumekuwa tukitumia gari moja ambayo tumeazimwa na Mgodi wa Williamson Diamond Limited.

Sasa Serikali inafanya jitihada gani za haraka kuhakikisha kwamba inapeleka angalau gari moja ya dharura kwa ajili ya kuokoa wananchi kupata huduma za msingi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Butondo, Mbunge wa Kishapu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Wilaya ya Kishapu inayochangamoto ya magari kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge, gari walilonalo ni chakavu, linahitaji matengenezo ya mara kwa mara. Nimpe matumaini Mheshimiwa Mbunge pale ambapo tutapata magari yanayotokana na bajeti hii tunayoitekeleza kipaumbele kitawekwa kule ambako hawana magari kabisa.

Kwa hiyo, kama Kishapu watakuwa hawana gari tutaelekeza IGP aipe Kishapu kipaumbele katika ugawaji wa magari hayo. (Makofi)