Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. KASALALI E. MAGENI K.n.y. MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuhakikisha upatikanaji wa mbegu bora za alizeti kwa wakulima ili kuzalisha mafuta ya kula?

Supplementary Question 1

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana na namshukuru pia Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri, lakini ninayo maswali mawili madogo ya nyongeza. Swali la kwanza; Serikali imekiri kwamba imeanza mchakato na inagawa mbegu bora za kilimo cha alizeti kwa wakulima. Je, ni lini sasa Serikali itahakikisha mbegu hizi zinafika kwenye Jimbo la Sumve kwenye Kata za Lyoma na Malya ambazo zimeonyesha uwezo mkubwa wa kuzalisha alizeti kuliko maeneo mengi ya nchi hii?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; uzalishaji wa mazao haya ya alizeti na upelekaji wa mbegu bora unategemea pia upatikanaji wa mbolea. Katika Jimbo la Sumve mbolea ya ruzuku ambayo tunaitegemea sana kwa mazao haya mpaka sasa haipatikani. Je, ni nini tamko la Serikali juu ya upatikanaji wa mbolea hii ya ruzuku ambayo imekuwa ni changamoto kubwa sana kwa wakulima wetu?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kasalali Mageni, Mbunge wa Sumve, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza kuhusu mbegu bora za alizeti kuwafikia wakulima wake, nikitoka hapa nakwenda kumpigia simu na kumwelekeza Mtendaji Mkuu wa ASA ahakikishe wakulima wa Sumve na wenyewe wanapata mbegu bora hii ya alizeti.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili kuhusu mbolea, ni kweli kumekuwepo na changamoto katika mfumo wa usambazaji, lakini tumeshatoa maelekezo kwa ndugu zetu wa CPB ambao wanashirikiana na wadau wengine kuhakikisha kwamba mbolea hii inawafikia wakulima kwa wakati. Kwa hiyo nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge, zilikuwepo changamoto, tumeendelea kuzifanyia kazi na muda sio mrefu CPB pamoja na mawakala wengine watasaidia ufikishaji wa mbolea kwa wakulima pasipo na usumbufu wowote kwa wakulima wetu wa Tanzania.

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. KASALALI E. MAGENI K.n.y. MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuhakikisha upatikanaji wa mbegu bora za alizeti kwa wakulima ili kuzalisha mafuta ya kula?

Supplementary Question 2

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa nini sasa Serikali isipeleke mbegu bure kabisa kwa wakulima wa alizeti ili waweze kuzalisha alizeti kwa wingi kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya mafuta hapa nchini?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Cherehani, Mbunge wa Ushetu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, dhamira ya Serikali ni kuona tunaongeza uzalishaji wa zao la alizeti, kila jambo linakwenda kwa hatua. Hatua ya kwanza tumeanza na ruzuku ya kuuza mbegu ya kilo moja kwa Sh.5,000 ambayo katika hali ya kawaida mkulima angepata kwa Sh.35,000 mpaka Sh.40,000. Kwa hiyo kwa hatua hii, ni hatua nzuri ambayo Serikali imeianza na huko mbeleni tutalifikiria ombi la Mheshimiwa Mbunge.