Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha wanawake wanakuwa wachimbaji wa madini nchini?

Supplementary Question 1

MHE. NEEMA G. MWANDABILA: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa wanawake ni kundi maalum ambalo linatakiwa kuwezeshwa na kutambuliwa kisheria katika sheria zetu mbalimbali, je, ni nini mkakati wa Wizara kuhakikisha wanawake wanaingia kisheria kwenye hii Sheria ya Madini.

Mheshimiwa Spika, pili, Songwe pia ni moja ya mikoa maarufu sana kwa uzalishaji wa madini; je, ni lini Serikali itakuja kuwapatia wanawake wa Mkoa wa Songwe mafunzo juu ya uchimbaji wa madini? Ahsante.

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Neema Gerald Mwandabila, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa swali lake la kwanza, Serikali inawatambua wanawake kipekee kabisa, siyo kama kundi maalum bali kama wadau muhimu katika sekta hii ya uchimbaji madini, na ndiyo maana tumeendelea kuwashirikisha wanawake katika mafunzo mbalimbali. Wizara imeendelea kuwafundisha faida za kushiriki katika uchimbaji wa madini, na imewahamasisha wajiunge kwenye vikundi ambavyo mpaka sasa hivi Tanzania tuna zaidi ya vikundi 20 vya wachimbaji wanawake na hata kule Songwe pia tumeendelea kuhamasisha na wapo wachimbaji wanawake wasiopungua 15.

Mheshimiwa Spika, kwa swali lake la pili, Wizara ina mkakati maalum wa kutoa mafunzo nchi nzima na baada ya Bunge hili taasisi zetu za GST, Tume ya Madini na STAMICO, wamepanga kwenda kutoa mafunzo katika Mkoa wa Songwe.