Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nancy Hassan Nyalusi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NANCY H. NYALUSI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua changamoto ya uhaba wa madaktari bingwa katika Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Iringa?

Supplementary Question 1

MHE. NANCY H. NYALUSI: Mheshimiwa Spika, pamoja na jitihada za Serikali, lakini hali bado ni mbaya.

Je, Serikali ina mkakati gani wa dharura wa kutatua changamoto hiyo?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, kama ambavyo Mheshimiwa Waziri wa Afya alieleza juzi hapa Bungeni, ni kwamba tunaendelea kuangalia sasa ikama ya madaktari kwenye hospitali zote za mikoa kwenye nchi yetu na kuwaangalia mabingwa kote waliko, tukiona na kuangalia hali ilivyo pale Hospitali ya Mkoa wa Iringa ili kuweza kuwahamisha maeneo mengine ambayo yamezidi na kupeleka kule Iringa.

Mheshimiwa Spika, lakini kuna masomo yanayoendelea miezi mitatu mitatu kwa ajili ya super specialists kwa hiyo tutawaondoa nao kwenye eneo hili na kuwasomesha kwa muda mfupi na kuwarudisha kwenye eneo hilo.

Name

Ghati Zephania Chomete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NANCY H. NYALUSI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua changamoto ya uhaba wa madaktari bingwa katika Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Iringa?

Supplementary Question 2

MHE. GHATI Z. CHOMETE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona.

Mheshimiwa Spika, changamoto iliyopo katika Hospitali ya Mkoa wa Iringa inafanana kabisa na changamoto iliyopo katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara. Je, ni lini Serikali itakwenda kutatua changamoto hii ya uhaba wa madaktari, hasa kwa magonjwa ya wanawake na watoto katika hospitali hiyo? Ahsante.

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa jinsi anavyofuatilia mambo ya mkoa wake, na nakumbuka alikuja Wizarani kwa ajili ya hilo. Ninamuomba Mheshimiwa Mbunge tukutane wakati wa haya mapitio ya kuwahamisha tuone tunaweza kufanya nini kwenye eneo la mkoa wake.