Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Robert Chacha Maboto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda Mjini

Primary Question

MHE. ROBERT C. MABOTO aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kumaliza mgogoro kati ya Wananchi na Wawekezaji wenye leseni ya uchimbaji madini Kata ya Guta – Bunda?

Supplementary Question 1

MHE. ROBERT C. MABOTO: Mheshimiwa Spika, nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, kati ya hawa 21 hawa Nane ndiyo wako kwenye source ya eneo lenyewe la uchimbaji, ndiyo maana hawajakubaliana na masharti ya wale Wawekezaji. Wizara ningewaomba wao wafanye kila linalowezekana ili kuwaweka vizuri, kwa sababu wale mashamba Nane waliobaki ni kwa sababu hawaoni kama wanapata haki zao zinazowastahili.

Swali la pili, ningeomba Mheshimiwa Waziri mara baada ya Bunge hili kuisha tuende nae mpaka kwenye eneo la tukio ili akajiridhishe yeye mwenyewe. Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Robert Chacha Maboto, Mbunge wa Bunda Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa swali lake la kwanza, kama nilivyokwishasema katika jibu langu la msingi, kwamba Mahakama imetoa fursa waendelee kujadiliana na endepo majadiliano hayo hayatazalisha ridhaa na wao waingie kwenye ubia kama wenzao, taratibu za kisheria, Sheria ya Madini Sura ya 123, Kifungu cha 97 kinachoeleza jinsi ambavyo suala la compensation, reallocation na resettlement, yaani fidia au kuhamishwa na kuwekewa sehemu mbadala au kujengewa makazi mengine utafuatwa kwa ushirikiano na Wizara ya Ardhi na Mthamini Mkuu wa Ardhi wa Serikali. Kwa hiyo, tumejipanga katika kuhakikisha kwamba maridhiano ama yafikiwe au sheria ifuatwe ili madini hayo yenye thamani katika maeneo hayo yaweze kuchimbwa na kunufaisha Taifa.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa swali lake la pili, ni mtu wa field sana niko tayari baada ya Bunge hili tutapanga ratiba pamoja nae, tuone siku muafaka ambayo naweza kufika ili tukashuhudie maeneo hayo na kumaliza mgogoro uliopo. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. ROBERT C. MABOTO aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kumaliza mgogoro kati ya Wananchi na Wawekezaji wenye leseni ya uchimbaji madini Kata ya Guta – Bunda?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Spika,
nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itawalipa fidia stahiki wananchi wa mitaa ya Mwasonga, Madege na Sharifu wanaoguswa na mradi wa uchimbaji wa madini ya mchanga kupitia Kampuni ya Nyati katika Wilaya ya Kigamboni.

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Faustine Ndugulile, Mbunge wa Jimbo la Kigamboni, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kuna kampuni ya uchimbaji wa madini ya mchanga mzito unaitwa heavy sands katika Jimbo lake, na kampuni husika inaitwa Nyati na hivi sasa ninavyojibu swali lake majedwali yote ya malipo ya fidia yameshakamilishwa, wapo watakofidiwa wapatao 1,198 na Mdhamini Mkuu wa Serikali ameshamaliza kazi yake na hivyo mpango wa malipo yao unaweza ukafanyika ndani ya miezi miwili ijayo. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Charles Muguta Kajege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. ROBERT C. MABOTO aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kumaliza mgogoro kati ya Wananchi na Wawekezaji wenye leseni ya uchimbaji madini Kata ya Guta – Bunda?

Supplementary Question 3

MHE. CHARLES M. KAJEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Naulizia kuhusiana na eneo la Bunda. Eneo lile limekua ni muhimu sana kwa maisha na uchumi wa wachimbaji wadogo wadogo katika Wilaya yetu ya Bunda.

Je, kwa nini Serikali isiende pale na kulikata lile eneo ili sehemu nyingine ibakie kwa wachimbaji wadogo wadogo.

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la rafiki yangu Mheshimiwa Charles, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wizara ya Madini, kazi yetu ni kusimamia Sera, Sheria na Kanuni. Wawekezaji wa machimbo ya madini wawe wa ndani au wa nje, kazi yetu ni kuwasimamia na inapotokea kwamba eneo lina maslahi mapana ya Kitaifa na wenye eneo wamegoma kabisa kutoa ushirikiano, tunachofanya ni kufuata sheria zilizowekwa za huo utaratibu unaobainishwa katika Kifungu cha 97 cha Sheria yetu ya Madini Sura ya 123, kwa kuangalia suala la fidia, suala la kuhamisha watu na kuwapangia makazi mengine kwa mujibu wa sheria ambayo inashirikisha Wizara ya Ardhi pia, Sheria ya Vijiji au Sheria nyingine inayohusika na masuala ya ardhi. Ahsante sana. (Makofi)