Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kassim Hassan Haji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanakwerekwe

Primary Question

MHE. HASSAN HAJI KASSIM aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kuitanua sehemu ya kusafirishia abiria wanaokwenda Zanzibar katika Bandari ya Dar es Salaam?

Supplementary Question 1

MHE. HASSAN HAJI KASSIM: Mheshimiwa Spika, ahsante sana na nashukuru kwa majibu ya Serikali. Hata hivyo, kwa kuwa utaratibu uliokuwepo sasa hivi, wa abiria ambao wanasafiri wanasubiria sana nje kabla ya kuingia ndani. Je, ni lini Serikali hii itatoa maelekezo ya wale abiria ambao tayari wana tiketi, wasisimame pale nje, waingie ndani moja kwa moja na kusubiria usafiri ndani?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hassan Haji Kassim, Mbunge wa Mwanakwerekwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba eneo ama jengo lilipo la kusubiria abiria pale Dar es Salaam Kwenda Zanzibar lina uwezo wa kubeba abiria 150 na jengo ambalo tutajenga litakuwa na uwezo wa kubeba abiria 400.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa hatua ambayo Serikali inachukua tunaweza ratiba maalum, mahususi kwa boti zote mbili ambapo boti ya kwanza kama ambavyo iko inaondoka saa moja asubuhi, boti ya pili itaondoka saa tatu na nusu, boti ya tatu itaondoka saa sita, nyingine saa nane mpaka saa kumi na mbili. Kwa abiria wote ambao wanakuwa nje na wana tiketi, hawa ndio wanatakiwa waingie kwenye jengo hili ili kuruhusu wasafiri kuliko mwingine yeyote kwa sababu eneo lile bado ni dogo. Kwa hiyo, ni maelekezo kwa Serikali kwa abiria wote, lakini pia wale wote wanaosimamia eneo hili.

Name

Asya Mwadini Mohammed

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HASSAN HAJI KASSIM aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kuitanua sehemu ya kusafirishia abiria wanaokwenda Zanzibar katika Bandari ya Dar es Salaam?

Supplementary Question 2

MHE. ASIA MWADINI MOHAMED: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Changamoto hii ambayo inaonekana kwa abiria wetu kwa upande wa Dar es Salaam hali kadhalika changamoto hii imejitokeza sana kwa upande wa Zanzibar. Je, Serikali ina mpango gani wa upanuzi wa Bandari ya Zanzibar ama kuijenga bandari mpya ili kupunguza changamoto hii kwa abira wetu?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa suala la Bandari ya Zanzibar ni suala ambalo lipo kwenye Wizara ya Wenzetu kule, tutawasiliana nao ili tuone namna gani ya kupanua ujenzi wa Bandari hii ya Zanzibar.

Mheshimiwa Spika, ahsante.