Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. YAHYA A. MHATA aliuliza: - Je, Serikali ina taarifa juu ya upatikanaji wa madini Nanyumbu na Je, wananchi wananufaikaje?

Supplementary Question 1

MHE. YAHYA A. MHATA: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nichukue nafasi hii kuishukuru sana Wizara kwa majibu mazuri.

Mheshimiwa Spika, ndani ya Wilaya yangu kuna vikundi vya vijana ambao wamejiunga pamoja katika shughuli mbalimbali za utafutaji na uchimbaji wa madini. Kuna vikundi kama Chugu, Chiswala na wanaapolo group, changamoto walionayo ni ukosefu wa vitendeakazi sahihi vya uchimbaji. Je, Wizara ina mpango gani wa kuwasaidia vijana hawa vitendea kazi ili nao waweze kupata mapato halali ya kuwezesha kujikimu kimaisha? (Makofi)

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Yahya Mhata, Mbunge wa Nanyumbu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Taasisi yake au Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), limeingia makubaliano na Taasisi za Kifedha hapa nchini, ikiwepo benki ya NMB, CRDB, KCB na Benki hizi zimeanza kutoa mikopo ya kuwawezesha wachimbaji wadogo. Hadi sasa zimeshatoa jumla ya Shilingi Bilioni 36 ambazo zimepopeshwa na inaendelea na jitihada ya kuzungumza na taasisi hizi ili waweze pia kutoa msaada wa vifaa.

Mheshimiwa Spika, vilevile Wizara inaendelea kuhakikisha uchimbaji mdogo unaendelea kurasimishwa nchini na katika mwaka wa fedha 2021/2022 tumeweza kutoa leseni za uchimbaji mdogo 6,000. Niendelee kumuomba Mheshimiwa Mbunge, kwamba ahamasishe vikundi katika Jimbo lake, wajipange na waweze kufuatila uwezekano wa kupata mikopo hiyo kupitia mabenki ambayo tumeingia makubaliano nao kupitia STAMICO. Ahsante sana. (Makofi)