Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza: - Je, ni lini Mamlaka ya Mji Mdogo Shirati katika Wilaya ya Rorya itaanza kufanya kazi kama Mamlaka kamili?

Supplementary Question 1

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi, nitakuwa na swali moja dogo tu la nyongeza. Kwa kuwa Mamlaka ya Mji Mdogo, mamlaka ambayo imeahidiwa kwa muda mrefu kwa zaidi ya miaka kumi sasa. Mwaka 2009 Waziri Mkuu aliyemaliza muda wake Mheshimiwa Mizengo Pinda, aliahidi; pia imetajwa kwenye awamu karibu tatu za Ilani ya Uchaguzi ya Chama changu cha Mapinduzi. Mwaka 2020 Mheshimiwa Waziri Mkuu aliyepo naye aliahidi kuanzishwa kwa Mamlaka ya Mji Mdogo. Nilitaka nijue tu Mheshimiwa Waziri kama yuko tayari sasa kuongozana nami kwenda kujiridhisha sababu hizi zinazosema kwamba uanzishwaji wake unacheleweshwa kwa sababu ya mapato ya ndani. Tuongozane ili twende kujiridhisha kwa kukaa na wataalam na Halmashauri ili tuweze kupata jibu la pamoja la uanzishwaji wa Mamlaka ya Mji Mdogo wa Shirati.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Jafari Wambura Chege, Mbunge wa Rorya kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, niko tayari na nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge ndani ya wiki mbili tutakaa na Baraza la Madiwani pamoja na Wakurugenzi katika Halmashauri yake, kuainisha na kutangua vyanzo vyote vya mapato ili tuone kama vinaweza kuhudumia ili mamlaka hii ndogo iweze kuanza.