Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza: - Je, ni lini mradi wa kufua umeme wa upepo na jua wa MW 100 utaanza rasmi katika Halmashauri ya Wilaya ya Singida?

Supplementary Question 1

MHE. ABEID R. IGHONDO: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru kwa kunipatia fursa. Pamoja na majibu haya ya Serikali ningeomba kujua, kwa kuwa mradi huu ni muhimu sana katika nchi yetu, pia umechukuwa muda mrefu sana bila kukamilika. Je, Serikali sasa ina mkakati gani mahsusi na wa ziada wa kuhakikisha mradi huu unaanza uzalishaji mara moja. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Abeid Ighondo Ramadhani, Mbunge wa Singida Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama tulivyosema Mkandarasi tayari amepatikana kwa ajili ya majadiliano lakini tumepata changamoto ndogo ya yeye kuhitaji vitu ambavyo havikuwemo kwenye masharti ya tenda ya zabuni. Tumeshafikia mwisho na msimamo wa Serikali ni kwamba hakutakuwepo na Government Guarantee kwenye mradi huu, bali akubaliane tufanye vile tulivyokubaliana tangu mwanzo.

Mheshimiwa Spika, akikubali Januari tutaanza kufanya kazi hii na asipokubali, Serikali sasa ishaamua kuendelea mbele na Zabuni hii mpya ili tuweze kuhakikisha tunampata Mkandarasi wa kufanya kazi hii kwa wakati. (Makofi)