Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO aliuliza: - Je, Serikali imejipangaje kutatua migogoro ya ardhi kati ya Wananchi na Wawekezaji wenye mashamba makubwa Kibaha Vijijini?

Supplementary Question 1

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwanza niikumbushe Serikali kwamba, kuna eneo la Soga kwenye shamba la Mohamed Enterprise tayari kulishakuwa na maelekezo ya ekari 500 kurudi Serikalini. Kwa kuwa, kuna changamoto mbalimbali zinazoendelea kusababisha kutokutekelezwa kwa agizo hilo.

Je, Waziri atakuwa yupo tayari kuambatana nami mara baada ya Bunge kwenda kusaidia kuondoa hizo changamoto zinazosababisha utekelezaji wa agizo hilo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, pale Kata ya Kikongo kuna mwekezaji anaitwa Trans-continental na shamba moja la UFC ambalo lipo mikononi mwa Serikali, kuna wananchi ambao wapo pale muda mrefu, wana miaka mingi, karibu 15 mpaka 20, na wawekezaji hao hawajaendelea.

Je, Serikali inatoa tamko gani kuwaruhusu wawekezaji hao kuendelea na shughuli zao? (Makofi)

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Michael Costantino Mwakamo, Mbunge wa Kibaha Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza kuhusiana na suala la Soga kwenye shamba la Mohamed Enterprise naafikiana nawe Mheshimiwa Mbunge kwamba tutakwenda kutatua kero hizi maana tunaambiwa yanayoendelea huko siyo mazuri sana.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili kuhusiana na jambo la trans- continental kule Kikongo na Waya mifugo, Mheshimiwa Mbunge nataka nikuhakikishie utayari wa Serikali, kwenda kushirikiana nawe kutatua kero hizi. Pili, katika Shamba la Waya, tutashirikiana na Wizara ya Mifugo kuhakikisha kwamba hatua zinazostahiki kufuatwa ili kukabidhiwa shamba hilo kama ambavyo Serikali iliamua nazo pia zinafuatwa. (Makofi)