Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: - Je, nini chanzo cha vifo kwa akinamama wanaojifungua kwa njia ya upasuaji siku chache baada ya upasuaji?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, ahsante, namshukuru Naibu Waziri wa Afya kwa majibu yake.

Kwa kuwa, umesema kwamba Wizara imekwishafanya ufuatiliaji wa hivyo vifo na sababu zake. Moja ya sababu ni kutokana na matatizo ya dawa za ganzi (nusu kaputi).

Je, kuna watumishi wa kutosha wa kutoa dawa za nusu kaputi katika vituo vyetu vya afya?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa mwaka 2021 ni asilimia 4.1 ya akina mama walipoteza maisha baada tu ya kujifungua kwa oparesheni. Je, kuna utafiti wowote ambao Wizara imeufanya ili kubaini sasa ni dawa gani ambazo zinasababisha akina mama wanapoteza maisha? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, moja, anauliza kama tuna uhakika wa kuwa na wataalam wa kutoa dawa ya nusu kaputi kwenye nchi. Juzi mlimsikia Mheshimiwa Waziri wa Afya akieleza kuhusu mkakati wa Rais wetu Samia Suluhu Hassan, ametoa Shilingi Bilioni Nane kwa ajili ya kusomesha wataalam 524 kwa mwaka huu. Mojawapo wa eneo lililoangaliwa ni eneo hilo ambalo kwa kweli kuanzia kwenye hospitali zetu za Wilaya kushuka chini kumekuwepo na watalaam wachache lakini kwa wanaomaliza chuo mwaka huu tutaenda kupunguza hilo tatizo kwa kiasi kikubwa sana.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali lake la pili baada ya uchunguzi wetu kwamba imegundulika nini na tunatakiwa kufanya nini kwenye eneo hilo la kupunguza vifo vya akina mama. Moja, ndiyo maana unaona kuna eneo hili la kusomesha, imefanyika kazi kubwa sana, lakini baada ya Serikali yetu kutoa zile fedha za tozo, vituo vya afya 238 vimejengwa kwa mwaka huu tu peke yake. Pia mwaka huu ambulance 663 zinaenda kununuliwa, nazo mnajua zitakavyokwenda kuweza kupunguza kwenye eneo hilo suala la vifo vya akina mama na watoto.

Mheshimiwa Spika, labda nimalize kwa kumjibu namna hiyo.