Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ahmed Yahya Abdulwakil

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Primary Question

MHE. YAHYA ABDULWAKIL AHMED aliuliza: - Je, ni lini ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ununuzi wa meli nane za uvuvi itatekelezwa?

Supplementary Question 1

MHE. YAHYA ABDULWAKIL AHMED: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri na ya kutia moyo katika ununuzi wa meli hii, naipongeza Serikali kidogo, nina swali moja la nyongeza.

Kwa vile ununuzi wa meli hizi utashirikisha Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, watafaidika wa meli mbili na mbili itafaidika Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo Tanzania Bara, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeshirikishwa katika hatua hizi za awali za manunuzi haya? Ahsante. (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, ushirikishwaji wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar upo wa kiwango kikubwa kabisa na jambo hili linaratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu ikishirikiana na Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais upande wa Zanzibar na Wizara zetu pia vilevile ya Mifugo na Uvuvi na Wizara ya Uchumi wa Bluu lakini na Mashirika yetu vilevile ya TAFCO na ZAFCO yote yanafanya kazi hii kwa pamoja. Kwa hiyo, nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Abdulwakil kwamba Serikali inashirikishwa ipasavyo. Ahsante.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. YAHYA ABDULWAKIL AHMED aliuliza: - Je, ni lini ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ununuzi wa meli nane za uvuvi itatekelezwa?

Supplementary Question 2

MHE. SALMA RASHID KIKWETE: Mheshimiwa Spika ahsante sana. Naipongeza Serikali kwa mpango kabambe wa ununuzi wa hizo meli nane na wataanzia na meli nne. Je, Serikali ina mpango gani kwa mikoa yetu miwili Mikoa ya Mtwara na Lindi juu ya upatikanaji wa meli hizi angalau moja ukizingatia kwamba kule kuna samaki wengi. Ahsante. (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Salma Kikwete, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mpango wa Serikali ni kuhakikisha kwamba meli hizi kwanza zitamilikiwa na Shirika letu la TAFCO kwa ubia na mashirika binafsi na kwa upande wa Mikoa ya Lindi na Mtwara na kwingine kote ambako shughuli za uvuvi zinafanyika, Serikali imekuja na mpango madhubuti wa kukopesha wavuvi ambapo boti zaidi ya 150 zitakopeshwa nchi nzima katika maeneo ambayo shughuli za uvuvi zinafanyika na tayari maelekezo na maombi mbalimbali tumekwishayapokea ili harakati na utaratibu wa kuweza kuwapata wenye sifa za kukopa mikopo hii zifanyike na hatimaye waweze kupata mikopo isiyokuwa na riba.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha, ahsante.