Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. EDWARD K. OLELEKAITA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Arusha – Simanjiro – Kiteto hadi Kongwa kilometa 430 itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami kama ilivyoahidiwa katika Ilani ya Uchaguzi (CCM) 2020 – 2025?

Supplementary Question 1

MHE. EDWARD K. OLELEKAITA: Mheshimiwa Spika, sana, na niseme wazi kabisa kwamba nashukuru sana majibu ya Serikali ni mazuri sana sana. Pamoja na hayo Mheshimiwa Waziri natarajia kwamba hiyo barabara mtaanza kujenga kutoka Kongwa, Kwenda Kiteto mpaka Arusha. Swali la nyongeza, ni lini hasa kwa mipango yenu, baada ya hii process ya kufungua tenda, ninyi mmepanga lini sasa ujenzi huu uanze, ni Novemba, Desemba, Januari? Ahsante sana.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE):
Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Edward Olelekaita, Mbunge wa Kiteto kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza niishukuru Serikali kwa kuipongeza Serikali kwa hatua ambazo inaendelea kuzichukua. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba dhamira ya Serikali ni kwamba taratibu zimeshaanza, na kama makampuni haya mojawapo litakidhi vigezo, litapewa hiyo zabuni, kwa hiyo taratibu za manunuzi zitaanza ili kuanza ujenzi huo kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. EDWARD K. OLELEKAITA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Arusha – Simanjiro – Kiteto hadi Kongwa kilometa 430 itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami kama ilivyoahidiwa katika Ilani ya Uchaguzi (CCM) 2020 – 2025?

Supplementary Question 2

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru, kwa kuwa barabara ya Mlowo Kamsamba, ina umuhimu mkubwa sana wa kiuchumi kwa wananchi wa Wilaya ya Mbozi pamoja na Momba. Naomba kufahamu sasa, ni lini ujenzi wa kiwango cha lami utaanza katika barabara hiyo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Juliana Shonza, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Songwe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Mlowo Kamsamba, imeshafanyiwa usanifu wa kina na Serikali inatafuta fedha ili barabara hiyo iweze kujengwa kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. EDWARD K. OLELEKAITA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Arusha – Simanjiro – Kiteto hadi Kongwa kilometa 430 itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami kama ilivyoahidiwa katika Ilani ya Uchaguzi (CCM) 2020 – 2025?

Supplementary Question 3

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, ni lini Serikali itajenga barabara ya kutoka Sale kuelekea Mto wa Mbu kwa kiwango cha lami, ukizingatia barabara hii ni muhimu kwa shughuli za utalii?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Valentine Magige, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Barabara ya Mto wa Mbu – Loliondo hadi Sale ni barabara ambayo tumeanza kujenga kipande cha Waswaswale na kipande kilichobaki tayari usanifu umekamilika na Serikali sasa inatafuta fedha ili kuijenga barabara hiyo yote kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. EDWARD K. OLELEKAITA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Arusha – Simanjiro – Kiteto hadi Kongwa kilometa 430 itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami kama ilivyoahidiwa katika Ilani ya Uchaguzi (CCM) 2020 – 2025?

Supplementary Question 4

MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza; barabara ya Makofia – Mlandizi – Manarumango mpaka Vikumburu, ni lini itaweza kujengwa kwa kiango cha lami? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Barabara ya Makofia – Mlandizi – Mzenga hadi Vikumburu ipo kwenye mpango wa kujengwa kwa kiwango wa lami.

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. EDWARD K. OLELEKAITA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Arusha – Simanjiro – Kiteto hadi Kongwa kilometa 430 itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami kama ilivyoahidiwa katika Ilani ya Uchaguzi (CCM) 2020 – 2025?

Supplementary Question 5

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kuuliza, Serikali imefikia wapi maandalizi ya ujenzi wa barabara kutoka Lumecha – Kitanda – Malinyi – Kilosa - Kwa Mpepo hadi Ifakara kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Vita Kawawa, Mbunge wa Namtumbo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja ambayo inaanzia Lumecha – Malinyi kuja Ifakara, ipo kwenye Mpango kama nilivyojibu kwenye swali la msingi; na jibu lake ni hilo hilo kwamba tayari wazabuni wameshaoneshwa, hiyo barabara, nayo imewekwa kwenye mpango wa EPC+F. Ahsante.