Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hassan Zidadu Kungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwalinda watumiaji wa cyanide kama mbadala wa zebaki?

Supplementary Question 1

MHE. HASSAN Z. KUNGU: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kuuliza swali dogo la nyongeza pamoja na majibu mazuri ya Serikali.

Mheshimiwa Spika, cyanide na mercury ni kemikali ambazo zote zina athari kubwa kwa maisha ya watumiaji. Lakini pia cyanide ndiyo ina gesi ambayo inatoa sumu kali ambayo inaweza kusababisha vifo kwa watumiaji ukilinganisha na zebaki.

Je, Serikali imetoa elimu kiasi gani kwa watumiaji wale ili kuepukana na madhara ambayo yanaweza kupelekea vifo kwa wachimbaji wadogo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili kwa kuwa upatikanaji wa cyanide ni mchakato mkubwa na unahitaji mtaji mkubwa lakini pia unahitaji kuwa kibali ili uweze kununua cyanide jambo ambalo linapelekea wachimbaji wadogo wakashindwa kuipata hiyo kemikali ya cyanide.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwawezesha wachimbaji wadogo ili waweze kuipata kwa gharama nafuu ambapo sasa waweze kufanya shughuli zao za kila siku kama walivyokuwa wanaitumia mercury ambayo ilikuwa inaweza kukamata kwa 0.1 ambapo kwa kila siku wanakuwa wanazalisha na kuweza kupata chakula chao cha kila siku kulinganisha na cyanide? (Makofi)

Name

Ummy Ally Mwalimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Answer

WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, nimshukuru sana Mheshimiwa Hassan Zidadu Kungu kwa maswali yake mawili mazuri hususan katika kuhakikisha tunawalinda wachimbaji wadogo wa madini na madhara ya matumizi ya kemikali hatarishi.

Mheshimiwa Spika, ni kweli wachimbaji wadogo huko nyuma na wengine hadi sasa wanatumia madini au mercury kwa Kiswahili zebaki ili waweze kuchenjua dhahabu ambayo wanatenganisha dhahabu, udogo na madini mengine. Lakini kimataifa nchi yetu inawajibika kusitisha matumizi ya zebaki kwa mujibu wa Mkataba wa Minamata. Kwa hiyo, ndomana saizi tunasisitiza matumizi ya cyanide.

Mheshimiwa Spika, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kwamba cyanide ni ghali ukilinganisha na zebaki, kwa hiyo wachimbaji wengi wadogo hawana uwezo wa kumudu. Tunaendelea kushirikiana na Wizara ya Madini kuhakikisha kwamba tunatoa elimu ya matumizi ya cyanide na namna ya kujikinga na madhara na watu wa madini wako hapa.

Mheshimiwa Spika, pia tumeshajenga vituo vya mfano kwa ajili ya wachimbaji wadogo kujifunza jinsi gani ya kutumia madini haya ya cyanide kwa wachimbaji wadogo, kwa mfano pale Rwamgasa, Mkoani Geita tumeweka kituo hicho, Katente pia Mkoani Geita na Itumbi, Mkoani Mbeya.

Mheshimiwa Spika, lakini nataka nikiri bado tunayo kazi kubwa ya kufanya kwa sababu bado wachimbaji wetu wadogo hawana elimu, lakini pia vifaa kinga vya kujikinga na madhara yatokanayo na madini haya hatari ya cyanide.

Mheshimiwa Spika, tutaendelea kwa kutumia mamlaka ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Wizara ya Madini pamoja na wenzetu wa OSHA kuhakikisha kwamba wachimbaji wadogo wanapata elimu pamoja na kujikinga na madhara ya madini haya.