Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hassan Seleman Mtenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka mawasiliano ya simu Kata ya Jangwani na Mtawanya Manispaa ya Mtwara Mikindani?

Supplementary Question 1

MHE. HASSAN S. MTENGA: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kupata nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Naibu Waziri niliongozana naye mwaka jana kwenda Mtwara kuangalia maeneo ambayo yana matatizo ya mawasiliano ikiwepo bandarini pale Mtwara, pale Mitengo kwenye Hospitali ya Rufaa.

Sasa nahitaji commitment ya Serikali, kwa kuwa tulishawahi kwenda na mwenyewe ukaangalia uhalisia. Ni lini sasa minara hii itapatikana kwenye maeneo husika? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hassan Seleman Mtenga, Mbunge wa Mtwara Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa tuliongozana na Mheshimiwa Mbunge kuangalia changamoto ya mawasiliano katika maeneo haya. Lakini tulitoa maelekezo kwa operator wote ambao wanatoa huduma ya mawasiliano katika maeneo haya ili kuweza kufanya optimization ili kutatua changamoto hii.

Mheshimiwa Spika, kwa vile Mheshimiwa Mbunge bado anaonesha kuna changamoto pale, basi tutatuma wataalam wetu ili waweze kufanya tathimini ili tujirizishe kama kuna uhitaji wa ujenzi wa minara katika maeneo hayo. Nakushukuru sana.

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka mawasiliano ya simu Kata ya Jangwani na Mtawanya Manispaa ya Mtwara Mikindani?

Supplementary Question 2

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, Naibu Waziri alifanya ziara jimboni Kata ya Jana na alipokuwa pale aliahidi ujenzi wa minara sita ambayo itajengwa Kata ya Mwakata, Kata ya Mwaluguru, Kata ya Chela, Kata ya Mega na Kata ya Runguya, Kijiji cha Nyangarata.

Mheshimiwa Spika, sasa swali langu ni lini utekelezaji huu utaanza?
Ahsante.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Iddi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa katika kata hizo tuliahidi na tayari zimeingizwa katika mpango wa utekelezaji wa miradi hiyo, na katika miradi ambayo inaongozwa na Mradi wa Tanzania Kidigitali ambao ni miradi 763 na katika minara hiyo 763 na maeneo ya Mheshimiwa Kassim Iddi yatakuwemo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge aendelee kusubiri ilimradi tu mchakato wa utangazaji wa tender utakapokamilika, ujenzi wa minara utaanza mara moja. Ahsante.

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka mawasiliano ya simu Kata ya Jangwani na Mtawanya Manispaa ya Mtwara Mikindani?

Supplementary Question 3

MHE. MASACHE N. KASAKA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kuweza kuniona.

Kijiji cha Shoga kilichopo Kata ya Sangambi, Kijiji cha Sipa Kata ya Kambekatoto na maeneo karibu yote ya Kata ya Upendo yana changamoto kubwa sana ya mawasiliano ya simu za mkononi; je, ni lini sasa Serikali itapeleka minara ili kumaliza changamoto hii? Ahsante. (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimejibu katika majibu yangu ya msingi ni dhamira ya Serikali kuhakikisha kwamba tunatatua changamoto ya mawasiliano ili Watanzania waendelee kutumia huduma ya mawasiliano katika biashara na mambo mengine.

Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia maeneo ya Mheshimiwa Masache ni kwamba yameingizwa pia katika utekelezaji wa Tanzania Kidigitali katika miradi 763. Nakushukuru.

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka mawasiliano ya simu Kata ya Jangwani na Mtawanya Manispaa ya Mtwara Mikindani?

Supplementary Question 4

MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, hali ya kukosekana mawasiliano ya simu katika Kata ya Jangwani, Manispaa ya Mtwara Mikindani inafanana kabisa na hali ya Kata ya Dutumi na Kwala kwa Kijiji cha Kimalamisale, Wilayani Kibaha, Mkoani Pwani.

Je, ni lini sasa Mheshimiwa Waziri utafanya ziara katika maeneo hayo ili kujionea hali halisi? Ahsante.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hawa Mchafu, Mbunge Viti Maalum - Pwani kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge alinijulisha siku mbili zilizopita kuhusu maeneo haya na mimi nikaenda kufuatilia katika utekelezaji wa miradi yetu kwa bahati nzuri maeneo ambayo ameyataja Mheshimiwa Mbunge tayari yako kwenye utekelezaji katika ile miradi 763.

Mheshimiwa Spika, kwahiyo, kama kutakuwa na uhitaji wa kwenda kufanya ziara basi sisi kama Serikali tuko tayari kufika katika maeneo yenye changamoto. Nakushukuru sana.