Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Latifa Khamis Juwakali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LATIFA KHAMISI JUWAKALI aliuliza: - Je, ni lini Serikali italipa fidia kwa wananchi waliopisha maeneo ya Jeshi kama Chejuu na Dunga, Zanzibar?

Supplementary Question 1

MHE. LATIFA KHAMIS JUWAKALI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, nikushukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri ambayo yanakwenda kuwatia moyo wananchi.

Kwa kuwa suala hili Wizara mmesema kwamba lipo katika mchakato na wananchi hawa bado sasa hivi wanaendelea kuwa na matumaini makubwa, lakini bado wanakosa kushiriki shughuli zao za kiuchumi ikiwa suala la kilimo, suala la ufugaji kwa sababu tayari walishafanyiwa tathmini.

Je, Serikali mnatoa kauli gani kwa wananchi hawa ili waendelee kuwa na matumaini?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, Mheshimiwa Waziri wananchi hawa itakapokuwa imetoka hiyo fidia; je, muda huo ambao mtakuwa tayari mmeitoa hiyo fidia inakwenda kuendana na thamani ya fedha katika kipindi hicho yaani value for money? Nakushukuru.

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Kusini Unguja, Mheshimiwa Latifa Khamisi Juakali kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia katika jibu la msingi tayari kuna majibu yanayowapa wananchi matumaini, niwaambie tu Mheshimiwa Mbunge wananchi waendelee kuwa na matumaini kwa sababu azma ya Serikali hii ni kuhakikisha kwamba tunaondosha migogoro yote ambayo inakabili baina ya vyombo vyetu vya ulinzi na wananchi; na ndiyo maana katika jibu la msingi tukasema kuna majadiliano yanaendelea baina ya SMZ na Jeshi la Wizara ya Ulinzi. Lakini pia tukasema kwamba tayari tumeshaomba fedha kwa ajili ya kuwalipa fidia. Kwa hiyo, Mheshimiwa ahakikishe watu wake wanaendelea kuwa na matumaini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kingine kikubwa ni kwamba tutahakikisha kwamba thamani zitakwenda kwa mujibu wa mali zao, ikiwa vipando, ikiwa nyumba, lakini Serikali haitawadhulumu, itahakikisha kwamba wanapata kile ambacho wanastahiki. Nakushukuru.