Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: - Je, ni kwa nini ugonjwa wa TB hauwezi kuonekana kwa mara moja unapompata mwathirika?

Supplementary Question 1

MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kutoa maswali yangu mawili ya nyongeza.

Kwa kuchelewa kuonekana TB Serikali ina mkakati gani ili kuepukana na masuala ya maambukizi? (Makofi)

Je, kuna mpango gani wa kutoa elimu kwa umma juu ya ugonjwa huu kwa kupitia warsha, semina au kongamano? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mwantumu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la kwanza anasema kwa sababu ugonjwa wa TB unachelewa kuonekana Serikali ina mpango gani wa kusaidia wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, moja ni utafiti, tayari nchi yetu kwa kushirikiana na vyuo vikuu mbalimbali duniani umefanyika utafiti kwenye Hospitali ya Kibong’oto iliyoko Wilayani Siha ambao ulitizama vinasaba vya TB ambavyo huko nyuma TB ilichelewa kugundulika sana kwa sababu wakati mwingine ukipima unamuona mtu ana TB, lakini ni TB mfu, sasa imegundulika kupitia Hospitali yetu ya Kibong’oto technic ambayo inatumia RNA kwa kutumia watafiti wetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, moja ni kwenye kutambua haraka, sasa hivi kuna vipimo ambavyo vimegundulika madaktari wazalendo wa Kitanzania kwa kushirikiana na Wamarekani wamegundua vinaweza kutambua mapema vimelea. Lakini ya pili, tunapeleka huduma chini sasa kwa bajeti ya mwaka huu kuna vituo 1,859 vinakwenda kuwezeshwa kuweza kupima, kuna ambulance na x-ray digital ambazo ni movable zinakwenda kuzungushwa kwenye nchi nzima ambavyo kila mkoa itakuwa na ya kwake kwa ajili kuzunguka kwenye jamii kusaidia.

Mheshimiwa Naibu Spika, pili, amesema warsha na kutoa semina, sasa hivi Serikali imenunua malori ambayo ni hospitali inayotembea ambayo ina x- ray yenye artificial inteligency ambayo inatembea kila mkoa na kutoa semina na kwenda kwa kongamano, kila mikutano na kuitisha wananchi, kupima pale pale na tiba kutolewa eneo lile lile. (Makofi)